• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • UTALII IRINGA
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Mwanasheria wa NEMC Benard Kongola (kulia) akikagua migomba iliyokatwa katika shamba la Tommy Diaries Farm

Posted on: May 3rd, 2017

KIKOSI KAZI KUNUSURU MTO RUAHA CHARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI AGIZO TOMMY DIARIES FARM


Na Dennis Gondwe, IRINGA


Kikosi kazi namba tatu cha kunusuru ikolojia ya mto Ruaha mkuu kimeridhishwa na utekelezaji wa agizo la kuondoa migomba isiyo rafiki kwa vyanzo vya maji katika shamba la mifugo la Tommy diaries lililopo wilayani Kilolo.

Kauli hiyo ilitolewa jana na wakili wa serikali mkuu kutoka baraza la Taifa la la hifadhi ya mazingira (NEMC), Benard Kongola baada ya kikosi kazi hicho kwenda kufuatilia utekelezaji wa agizo la tarehe 24/4/2017 lililomtaka muwekezaji huyo kuondoa migomba hiyo shambani kwake wilayani kilolo.

Migomba iliyokatwa.

Kongola alisema “migomba ambayo si rafiki kwa vyanzo vya maji ilikuwa imepandwa ndani ya mita 60 kutoka kingo za mto Ruaha mdogo jambo ambalo ni ukiukwaji wa sheria ya Mazingira ya mwaka 2004, sehemu ya 57 ibara ndogo ya 1 inayozuia kulima au kufanya shughuli za kibinadamu ndani ya mita 60”. Alisema kuwa walipotembelea shamba hilo kukagua hali ya uhifadhi wa mazingira na ikolojia ya bonde la mto Ruaha mkuu waligundua uharibifu huo wa kimazingira na pamoja na kuwapiga faini ya shilingi milioni 10 kutokana na kulima mahindi na migomba ndani ya hifadhi ya mto na waliwataka kuondoa mazao hayo yaliyolimwa ndani ya mita 60.

Migomba iliyokatwa

Migomba iliyokatwa

Wakili Kongola alizitaka mamlaka za serikali za mitaa kusimamia sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 kwa sababu ipo wazi. Alisema kuwa usimamiaji makini wa sheria hiyo utasaidia kudhibiti shughuli za kibinadamu zinazofanyika ndani ya mita 60 katika nyanzo vya maji jambo linalohatarisha uendelevu wa vyanzo hivyo wilayani Kilolo.

Ikumbukwe kuwa shamba la mifugo la Tommy diaries lilipigwa faini ya shilingi milioni 10 kutokana na kulima mahindi na migomba ndani mita 60 kutoka ukingo wa mto Ruaha. Vilevile, shamba la mifugo la Ndoto pia lilipigwa faini ya shilingi milioni 10 kutokana na kufanya biashara bila kuwa na cheti cha tathmini ya Mazingira (EIA).

=30=



Matangazo

  • JOINING INSTRUCTION SHULE ZA SEKONDARI ZA SERIKALI MKOA WA IRINGA 2021 December 15, 2020
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA IRINGA 2021 December 18, 2020
  • Ratiba ya Mhe. Mkuu wa Mkoa kwa Mwezi Machi March 08, 2019
  • Ratiba ya Mh. Mkuu wa Mkoa kwa Mwezi Aprili April 04, 2019
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkuu wa Mkoa Ally Hapi na Katibu Tawala Mkoa Bi, Happiness Seneda, pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama

    June 11, 2020
  • Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Ally Hapi Aongoza Mkutano wa Baraza la Madiwani Kujadili Hoja za Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) Halmashauri ya Wilaya Mufindi Tarehe 28 Mei, 2020

    May 28, 2020
  • Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Ally Hapi Aongoza Mkutano wa Baraza la Madiwani Kujadili Hoja za Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) Halmashauri ya Mji wa Mafinga Tarehe 22 Mei, 2020.

    May 22, 2020
  • Mh. Hapi aongoza kikao kujadili Hoja za Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) Halmashauri ya Wilaya ya Iringa

    May 15, 2020
  • Tazama zote

Video

Wanasiasa uchwara wanapotosha jamii kuhusu corona
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Pawaga Road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, Iringa

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2019, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.