• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

WILAYA YA KILOLO YATAKIWA KUHAMASISHA JAMII KUJENGA MIUNDOMBINU YA ELIMU

Posted on: July 3rd, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Watalaam wa sekta ya elimu wilayani Kilolo wametakiwa kuielimisha na kuihamasisha jamii kuunga mkono juhudi zinazofanywa za kujenga miundombinu ya elimu kwa lengo la kukuza utoaji wa huduma hiyo.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua kikao cha wadau wa maendeleo ya sekta ya elimu wilaya ya Kilolo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya ya Kilolo.

Masenza alisema kuwa shule wilayani Kilolo zinachangamoto ya miundombinu, utoaji wa chakula cha mchana na usimamizi makini wa utekelezaji wa sera ya elimu. “Sote kwa pamoja tunawajibika kuihamasisha jamii juu ya kuchangia maendeleo ya taasisi zetu za kielimu. Jukumu la kuhakikisha shule zetu zina miundombinu madhubuti ni la jamii inayotuzunguka kwa ubia na serikali yetu ya awamu ya tano. Wajibu wetu ni kuielimisha jamii juu ya hili na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na jamii” alisema Masenza. Yapo maeneo ambayo yamefikia mafanikio makubwa, ambayo yanatakiwa mafanikio hayo kuambukizwa maeneo ambayo hayafanyi vizuri, aliongeza.

Mkuu wa Mkoa aliwataka wadau wa maendeleo ya sekta ya elimu wilaya ya Kilolo kuchambua na kushirikishana mipango itakayoleta maendeleo thabiti katika sekta ya elimu. Aidha, aliwataka kujenga ari ya ushindani na kupigania nafasi za ushindani wa juu zaidi katika kufikia mafanikio ya sekta ya elimu. Aliwataka kutumia kikao hicho kuongeza juhudi na ubunifu utakaosaidia kutatua changamoto na kuongeza ufanisi katika kuendeleza sekta ya elimu.

Kikao cha wadau wa sekta ya elimu Wilaya ya Kilolo kinalenga kuwakumbusha wajibu katika kufikia mafanikio ya sekta ya elimu pamoja na kushirikishana changamoto na kujadili suluhisho la pamoja.

=30=


Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU ASHIRIKI MBIO ZA GRUMA 2025

    July 05, 2025
  • KUELEKEA MBIO ZA THE GREAT RUAHA MARATHON

    July 01, 2025
  • MAAFISA ELIMU WAAGIZWA KUSIMAMIA MAENDELEO YA MICHEZO MASHULENI

    June 29, 2025
  • MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 YACHAGIZA UCHUMI WA IRINGA.

    June 29, 2025
  • Tazama zote

Video

MAENDELEO KWA SASA BILA MAWASILIANO HAYAWEZEKANI- RC KHERI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.