• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Video

  • RC: SERUKAMBA AWAPA SIKU SABA TAKUKURU KUCHUNGUZA MIRADI YA IRINGA DC

    April 11th, 2024

    Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba amemuagiza kamanda Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoa wa Iringa kufanya uchunguzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kukagua Nyumba ya Mkurugenzi, hospitali ya wilaya,nyumba za watumishi Pamoja na ukarabati wa ukumbi wa siasa ni kilimo

    Hayo yamejiri leo wakati wa Mhe. Serukamba alipotembelea katika Halmashauri hiyo na kukutana na madiwani na wataalamu ambapo baadhi ya madiwani wamesema kuwa kumekuwa na udanganyifu katika ujenzi wa baadhi ya maeneo.

    Mhe.Mathew Singanyagwa ni Diwani wa kata wa Masaka ametoa ya moyoni na kusema kuwa suala la ukumbi wa siasa ni kilimo ni ukumbi wa muda mrefu sana na kwamba katika ukarabati wake umefikia asilimia Hamsini si sahihi na hizo nyumba za watumishi kwasasa bado ni mapagala

    Mhe. Fundi Mihayo diwani wa kata ya Ilolo mpya amesema kwa sasa Halmashauri hiyo haiko vizuri sana kwani katika hospitali ya Wilaya mpaka sasa kuna majengo nane hayajakamilika na pesa tayari Serikali imekwisha kutoa hivyo amemuomba Mkuu wa Mkoa kulishughulikia hili suala

    Nae Mhe. Yohanes Mlusi amesema kuwa wao kama madiwani ndio wasimamizi wakuu wa kuhakikisha miradi ya Serikali inakwenda lakini kumekuwa na changamoto ya wao madiwani kutosikilizwa pale wanapo shauri kwa wataalamu mambo ya kufanya

    Akizungumza baada ya kuwasikiliza madiwani hao Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba amesema kufikia jumatatu ya wiki ijayo anahitaji majibu kutoka kwa takukuru juu ya miradi ya ujenzi wa majengo ya Hospitali ya wilaya,nyumba za watumishi,ukuta wa wigo wa jengo la Halmashauri na ukumbi wa siasa ni kilimo

    “na Takukuru nataka unisaidie jambo moja tumeambiwa ukumbi huu haukarabatiwa lakini kuna hela za ukarabati zimewekwa nataka uthibitishe tunakarabati au la,nataka uniletee ripoti juu ya uzio huo ulioanguka kuhusu nyumba hiyo ya Mkurugenzi lakini pia kuhusu Hospitali ya Wilaya nataka hiyo ripoti tujue”

    Aidha Mhe. Serukamba amewataka wahasibu kwenye Halmashauri kuachana na tabia ya kukaa na fedha zilizotoka Serikali kuu na badala yake amesema fedha hizo pindi zinapofika wahakikishe wanazipeleka kwenye miradi husika.

    Pia ameongeza kwa kusema kuwa kwa sasa watashughulika na wabadhirifu wote wanaorudisha maendeleo nyuma kwa kujinufaisha wao binafsi hivyo wananchi waendelee kuwa na Imani na Serikali yao.

    Sambamba na hayo mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Stephen Mhapa ameahidi kushirikiana bega kwa bega na Mkuu wa Mkoa na wengineo kuhakikisha wanaendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuleta maendeleo katika mkoa wa Iringa.

  • WANANCHI WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA UWEPO WA MAONYESHO YA KARIBU KUSINI 2023

    September 22nd, 2023


    Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Halima Dendego Amewataka Wananchi wote Kutumia Fursa ya Maonyesho ya Utalii Karibu Kusini Yatakayofanyika Katika Viwanja vya Kihesa Kilolo Kuanzia Tarehe 23 hadi 27/09/2023.

    Ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake ambapo amesema kuwa lengo la maonyesho hayo ni pamoja na kuiishi kampeni ya The Royal Tour ilioanzishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Pamoja na kutangaza fursa za utalii na uwekezaji zilizopo kusini mwa Tanzania.

    Mikoa Kumi ya Kusini mwa Tanzania Inataraji Kushiriki Maonyesho Hayo yenye Hadhi ya Kimataifa


    Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa


  • MAONESHO YA KIMATAIFA YA UTALII KARIBU KUSINI 2023

    September 22nd, 2023
  • ← Prev
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • Next →

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KARIBU MWENGE WA UHURU MKOA WA IRINGA 2025

    April 13, 2025
  • KARIBU MWENGE WA UHURU MKOA WA IRINGA 2025

    April 03, 2025
  • RAIS DKT. SAMIA ATOA MKONO WA HERI KWA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM IRINGA

    March 30, 2025
  • LAAC YAIELEKEZA OFISI YA MKUU WA MKOA IRINGA KUIMARISHA USIMAMIZI WA MIRADI.

    March 18, 2025
  • Tazama zote

Video

WASHIRIKI 10,000 KUTIKISA MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 MKOANI IRINGA
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

Tovuti Linganifu

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.