• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

KIWANDA CHA KARATASI MUFINDI CHATAKIWA KUZALISHA KARATASI NYEUPE

Posted on: September 9th, 2018

Serikali ya Mkoa wa Iringa imekiagiza kiwanda cha karatasi Mufindi (MPM) kuanza kuzalisha karatasi nyeupe ili kuongeza ajira kwa vijana na mapato ya Serikali.

Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi alipokuwa akiongea na menejimenti ya kiwanda hicho baada ya kufanya ziara ya kukikagua jana.

Mhe Hapi alikiagiza kiwanda hicho kuanza kutengeneza karatasi nyeupe zinazotumika katika shajala mbalimbali kwenye ofisi na madaftari. Alisema kuwa wakati wa kukagua kiwanda hicho, amekuta mashine za kutengeneza karatasi nyeupe zimezimwa jambo linaloikosesha Serikali mapato. “Ndugu zangu, uzalishaji wa karatasi nyeupe katika kiwanda hiki utasaidia kuongeza ajira kwa vijana wetu, utapunguza gharama kubwa ya kununua karatasi nyeupe na kuongeza mapato ya Serikali. Hiki ni kiwanda kikubwa kilichokuwa kinategemewa na nchi.” alisema Mhe Hapi.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa eneo la kiwanda hicho lina uwekezaji mkubwa uliofanywa na Baba wa Taifa Mwl Julius Nyerere katika awamu ya kwanza ya utawala wake. “Serikali ya Mkoa inataka kubaini malengo ya Baba wa Taifa aliyokuwa nayo katika kiwanda hiki hadi mataifa mbalimbali yalikuwa yanakuja kujifunza katika kiwandani hapa. Nataka kujua masharti yaliyotolewa na Serikali wakati wa ubinafsishaji kama yametekelezwa na muwekezaji” alisema Mhe Hapi.

Vilevile, alishangazwa na reli ya TAZARA sehemu ya mchepuko wa kuingia kiwandani hapo kutokufanya kazi kwa muda mrefu. Alisema kuwa malengo ya Serikali kwa reli hiyo yalikuwa kurahisisha na kupunguza gharama za usafirishaji wa karatasi kutoka kiwandani hapo kuelekea maeneo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Kiwanda cha karatasi Mufindi kilibinafsishwa mwaka 2004 kikiwa na uzalishaji wa karatasi nyeupe na karatasi ngumu kikiwa na uwekezaji uliofanywa na Baba wa Taifa wa dola za kimerekani milioni 360.

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.