• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

BENKI YA MUCOBA KUKOPESHA BILIONI 5 WAKULIMA

Posted on: June 26th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Benki ya MUCOBA imepanga kutoa mikopo ya kilimo zaidi ya shilingi bilioni tano katika kuunga mkono juhudi za Rais Dkt John Magufuli za kuendeleza sekta ya kilimo nchini.

Kauli hiyo ilitolewa na meneja mkuu wa benki ya MUCOBA, Ben Mahenge alipokuwa akisoma taarifa ya benki hiyo katika hafla ya uzinduzi wa mfumo wa stakabadhi ghalani katika Tarafa ya Pawaga wilayani Iringa.

Mahenge alisema “mheshimiwa mgeni rasmi, kwa mwaka 2018 benki imepanga kutoa mikopo ya kilimo yenye thamani ya shilingi bilioni 5.052”. Alisema kuwa lengo ni kuwawezesha wakulima kuzalisha kwa wingi, na kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. John Magufuli ya kuongeza kipato kwa wakulima. Mwaka jana benki ilianzisha mikopo inayoitwa wakulima Digital kwa ushirikiano wa AGRA na SELF, alisema. Mikopo hiyo hutolewa kwa awamu tatu kwa mkulima. Alizitaja awamu hizo kuwa ni wakati wa maandalizi ya shamba, wakati wa kilimo na kupalilia na wakati wa kuvuna.

Akiongelea faida za mikopo hiyo, alizitaja kuwa ni kupunguza usumbufu na muda wa kupata mkopo, kupunguza gharama za kufuata mkopo kwenye vituo na kutunza siri za wateja. Faida nyingine alizitaja kuwa ni usalama wa wateja kuimarishwa na kupunguza matumizi yasiyo lengwa.

Meneja huyo alisema kuwa benki yake iliona ni jambo jema kutoa mikopo ya stakabadhi ghalani hasa kipindi cha mavuno. Lengo ni kuwawezesha wakulima kuweza kupata fedha ya kuvunia na kujikimu katika kipindi ambacho watakapo kuwa wametunza mazao yao ghalani wakisubirishia bei ya mazao yao kuongezeka sokoni ili waweze kuuza kwa bei nzuri, alisema.

Akiongelea changamoto ya dhamana kwa wakulima, alisema kuwa wakulima wengi hawana dhamana na kusema kuwa dhamana ya wakulima itakuwa mazao yao yatakayokuwa yametunzwa gharani.

Ikumbukwe kuwa benki ya MUCOBA imejikita kuwahudumia wananchi wa kipato cha chini hasa wakulima ikiwa imetoa mikopo ya kilimo kiasi cha shilingi bilioni 11 kwa mwaka 2015, 2016 na 2017.

=30=



Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.