• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

HALMASHAURI NYANDA ZA JUU KUSINI ZATAKIWA KUPELEKA HUDUMA ZA UPIMAJI AFYA KATANI

Posted on: August 16th, 2017

Mamlaka za serikali za mitaa mikoa ya nyanda za juu kusini zimetakiwa kuweka utaratibu wa kupima afya katika Kata ili wananchi wengi wanufaike na huduma za afya na kukabiliana na magonjwa.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipotembelea banda la Halmashauri ya wilaya ya Kilolo katika maonesho ya Nanenane kwenye uwanja wa John Mwakangale mjini Mbeya jana.

Masenza alizitaka Halmashauri kuweke utaratibu wa kutembelea Kata na kutoa elimu ya afya na upimaji magonjwa mbalimbali badala ya kusubiri kupima katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika mara moja kila mwaka. “Wekeni utaratibu wa kutembelea Kata na kupima afya wananchi hasa wakina mama wanapohudhuria kliniki na kuwapa elimu ya afya na lishe. Utaratibu huu utasaidia kuokoa maisha ya watu na kuimarisha hali zao za lishe kwa sababu wananchi wengi hawapati huduma hizo kutokana na sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na umbali” alisema Masenza. 

Masenza alisema kuwa mikoa ya nyanda za juu kusini inakabiliwa na tatizo la lishe pamoja na kuwa ni mikoa yenye kiwango kikubwa cha uzalishaji wa mazao ya chakula. Alizitaka mamlaka za serikali za mitaa na wadau wote kuweka mikakati ya kuhakikisha elimu inaendelea kutolewa kwa wananchi juu ya uchanganyaji wa chakula katika kutengeneza mlo kamili. “Juhudi za pamoja zitasaidia kukusanya rasilimali na kuzitawanya kwa mujibu wa maeneo ya kipaumbele na uhitaji kuliko kila mmoja kufanya peke yake. Ushirikiano huu utarahisisha kuzibaini changamoto zilizopo na kuzipatia ufumbuzi wa pamoja” alisema Masenza.

Maonesho ya shughuli za wakalima Nanenane mwaka 2017 yanaongozwa na kaulimbiu isemayo, “zalisha kwa tija mazao na bidhaa za kilimo, mifugo na uvuvi kufikia uchumi wa kati”.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.