• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

HISTORIA YAANDIKWA BARABARA YA KWENDA HIFADHI YA RUAHA - ZAIDI YA BILLION 142 KUKAMILISHA MRADI HUO

Posted on: September 21st, 2024

Mamia ya wakaazi wa Mkoa wa Iringa Wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba Leo September 21, 2024 wameshuhudia tukio la kihistoria la utiaji saini mkataba wa ujenzi wa barabara ya lami yenye Km. 104 kutoka Iringa Mjini hadi Hifadhi ya Taifa ya Ruaha

Barabara hiyo ya Iringa- Msembe itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami ikiwa ni mchakato uliochukua takribani miaka 60 hadi utekelezaji wake.

Hafla ya utiaji saini kwa mkataba wa ujenzi wa barabara hiyo baina ya Wakala wa Barabara Tanzania(TANROADS) na kampuni ya China Henan International Company Limited (CHICO)  imefanyika katika uwanja wa Samora, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.

Akizungumza katika hafla hiyo Waziri wa Ujenzi Mhe.Innocent Bashungwa (Mb) amesema kuwa mkataba wa ujenzi wa barabara ni mafanikio makubwa kwa Tanzania hasa katika kuinua sekta ya utalii na Uchumi Mkoani Iringa.

Aidha Mhe.Bashungwa amewahikikishia wananchi wanaodai fidia ya kupisha ujenzi wa barabara hiyo kuwa watalipwa stahiki zao kwa wakati baada ya tathimini kumalizika.

Akitoa maelezo ya barabara hiyo Mtendaji mkuu wa TANROADS Eng. Mohamed Besta amesema kuwa ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa Kilometer 104 utachukua miezi 24 ikigharimu kiasi cha shilingi bilioni 142.56

Akitoa salaamu za Mkoa Mhe. Serukamba ametoa shukrani kwa Serikali huku akiiomba Wizara hiyo kushughulikia kwa haraka suala la fidia.

Kusainiwa kwa mkataba wa ujenzi wa barabara hiyo kumepongezwa na wabunge wa Mkoa wa Iringa waliohudhuria katika hafla hiyo akiwemo Mhe. William Lukuvi (Isimani), Mhe. Jesca Msambatavangu (Iringa mjini), Mhe. Jackson Kiswaga (Kalenga) na wabunge wa viti maalum Mhe. Nancy Nyalusi na Mhe. Rose Tweve ambao  wametaja kama historia kwa mkoa huo na kusema kuwa Serikali imelipa deni kubwa kwa wananchi wa Iringa.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.