• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Mhe Ally Hapi, Mkuu wa Mkoa Iringa, amefanya ziara ya kutembelea Tarafa ya Idodi

Posted on: January 28th, 2020

Mhe Ally Hapi, Mkuu wa Mkoa Iringa, amefanya ziara ya kutembelea Tarafa ya Idodi na Kata ya Nzihi na kujionea uharibifu uliofanywa kutoka na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha Mkoani Iringa.

Akiwa katika Ziara hiyo Mhe Ally Hapi, alianza kujionea daraja la Nzihi amabalo limebomoka kingo za pembeni mwa daraja hilo na kupelekea kuatarisha maisha ya wasafiri wanatumia njia hiyo, hivyo magari yote yanapita upande mmoja, lakini hata sasa Tanroads wapo kazini kwa ajili ya kutengeneza kingo hizo ili kuzuia daraja hilo lisibomoke.

Baadae Mhe Hapi, na kamati ya Ulinzi na Usalama waliekea katika kituo cha Afya Idodi kwenda kumfariji Bi, Akhadija Keyela, Mkazi wa Kitisi ambaye amefiwa na watoto wake 2 wa kiume ambaye ni Bosko Keyele (8) na Stivini Keyele (5) watoto hao walisombwa na maji wakiwa shambani na mama yao aliyekuwa akiangalia mazao yake. Bi, Akhadija alikuwa na watoto wake 4 shambani  ambapo watoto 2 aliwaokoa.

Akiwa Idodi alienda kijiji cha Tungamalenga ambapo aliona uharibifu mkubwa wa miundombinu ya barabara pamoja na  daraja linalounganisha mbuga ya Ruaha National Park na kijiji cha Tungamalenga. Na baadae alishiriki katika zoezi la ugawaji wa vifaa kwa wahanga waliokumbwa na mafuriko Idodi, msaada huo umetolewa na Redcross pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Iringa wenye thamani ya Milion 4,116,500, vifaa hivyo ni magodoro 30,unga kilo 200, maharage kilo 100, blanket 30, ndoo za lita ishirini 15, madumu ya lita ishirini 15, vifaa vya akina mama 15, vifaa vya jikoni 15.


Mhe Hapi, akiwa kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Idodi, amewataka wa Nchi wote wa mkoa wa iringa kuchukua tahadhari na mvua zinazoendela kunyesha, “ amesema kwa mujibu wa taarifa za mamlaka ya hali ya hewa mvua zinazotarajiwa kunyesha ni kubwa sana” hivyo ni vema wananchi wakachukua taadhari mapema. Amewataka wale wote waliojenga mabondeni kuhama haraka sana, walioko mashambani pia nao wasiende kwa kipindi hiki maana hali ya hewa si nzuri sana, na wazazi kuwa makini na watoto wao hasa wanapoenda shule na kurudi majumbani wawafatilie ili wasije wakasombwa na maji, lakini pia amewaonya na walevi wa ulanzi kuwa makini kipindi hiki cha mvua wanywee majumbani au kuacha kabisa na amewataka Wananchi wote wa Mkoa wa Iringa hususani waliokumbwa na mafuriko wachemshe maji ya kunywa ili kuepukana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.

Imetolwa na Afisa Habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa

Humphrey Kisika.


Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.