• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

MIRADI YA MAENDELEO YENYE DHAMANI YA ZAIDI YA BILLIONI 30 KUPITIWA NA MWENGE WA UHURU MKOA WA IRINGA

Posted on: April 24th, 2025

Miradi ya Maendeleo ya Zaidi ya Bilioni 30 Kupitiwa na Mwenge wa Uhuru Iringa

Zaidi ya miradi ya maendeleo 46 yenye thamani ya shilingi bilioni 30.8 inatarajiwa kukaguliwa na Mwenge wa Uhuru mwaka huu katika Mkoa wa Iringa, ambao utakimbizwa umbali wa kilometa 625.1 kuanzia tarehe 28 Aprili hadi 3 Mei 2025.

Akizungumza na waandishi wa habari leo April,24,2025 mjini Iringa, Mkuu wa Mkoa wa Iringa,Mhe. Peter Serukamba, amesema kuwa Mwenge wa Uhuru utaanza mbio zake mkoani humo ukitokea Mkoa wa Dodoma mnamo Aprili 28, 2025 kuanzia saa 12 asubuhi.

Kwa mujibu wa Mhe. Serukamba, amesema kuwa mwenge huo utakimbizwa katika halmashauri zote tano za Mkoa huo ambazo ni Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Kilolo, Mufindi, Halmashauri ya Mji Mafinga na Manispaa ya Iringa.

“Mwenge huu si tu unakuja kuhamasisha maendeleo bali pia kuhimiza mshikamano wa kitaifa, amani na uwajibikaji kwa viongozi na wananchi,” amesema Serukamba.

Ratiba ya mbio za Mwenge mkoani hapa  itahitimishwa Mei 3, 2025 katika Uwanja wa Michezo wa Shule ya Msingi Idofi, ambapo sherehe ya makabidhiano ya mwenge kati ya mikoa ya Iringa na Njombe itafanyika.

Miradi itakayozinduliwa, kukaguliwa na kuwekewa mawe ya msingi inajumuisha ile inayotekelezwa katika sekta muhimu kama afya, elimu, maji, lishe, miundombinu pamoja na miradi ya uzalishaji mali inayolenga kuongeza kipato cha wananchi wa kawaida.

Aidha, Serukamba ametoa wito kwa wananchi wa Iringa kujitokeza kwa wingi kuupokea Mwenge wa Uhuru na kushiriki kikamilifu kwenye shughuli zitakazoambatana na Mwenge wa Uhuru, akisisitiza umuhimu wa kudumisha amani, utulivu na mshikamano wakati wote wa tukio hilo.

Kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka huu ni "Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu" ikilenga kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika mchakato wa kidemokrasia kwa njia ya amani,” 

Mbio za Mwenge wa Uhuru hutoa fursa ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kutambua changamoto zilizopo, na kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za kijamii na kiuchumi.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.