• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa Iringa atoa maagizo mazito kwa Jamii Kupambana na Ukatili kwa Wanawake na Watoto

Posted on: January 16th, 2020

Mkuu wa Mkoa Iringa atoa maagizo mazito kwa Jamii Kupambana na Ukatili kwa Wanawake na Watoto, Atoa Maelekezo kwa Wakuu wa Wilaya na Wadau Mbalimbali

Akitoa maelekezo hayo katika kikao kilichoandaliwa na Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Jinsia na Wanawake na Watoto, Mheshimiwa Ally Hapi amesema, kuna umuhimu wa kupitia upya waganga wote wa jadi waliopo Mkoani humo, kuacha mila na desturi zilizopitwa na wakati, kuacha mambo ya kishirikina na ulevi wa kupindukia.

Mheshimiwa Hapi amesema mambo haya huchangia sana kufanya ukatili kwa wanawake na watoto. Akitoa mfano akasema mwanaume akishalewa anaweza kumpiga mke wake bila sababu. Utamaduni wa kupiga mwanamke umepitwa na wakati, mwanamke anatakiwa kupewa mapenzi, kubembelezwa na kupewa mahaba. Pia mtu akishaenda kwa mganga wa jadi kutafuta utajiri, ataambiwa akabake mtoto.

Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Watoto wameandaa mpango unaoitwa MTAKUWWA, ambao unafadhiliwa na UNICEF, mpango huu wa mawasiliano utasaidia kupunguza ukatili kwa wanawake na watoto. Pamoja na jitihada za UNICEF lazima jamii ipewe elimu juu ya mambo haya ya ukatili wa wanawake na watoto.

Ameongeza kuwa, hata wanaume huwa wanafanyiwa ukatili japo huwa hawasemi. Pia wazazi hatuna desturi za kuangalia watoto wetu pindi wanapotoka shule au kucheza sehemu mbalimbali. Kwani imebainika kuwa asilimia kubwa watoto hubakwa, kulawitiwa wakiwa wanatoka kwenye masomo ya ziada (Tuition), vibanda wanavyoonesha sinema na hata kumtuma mtoto nyakati za usiku kwenda dukani au sehemu mbalimbali.

Amesisitza tena, kila shule kuwe na mwalimu wa malezi ambaye atakuwa akiwaangalia na kuwasikiliza watoto pindi wanapokuwa wamepatwa na jambo kama hili. Hii itasaidia watoto kueleza matatizo yao bila uoga.

Ameongeza kwa kusema kuwa, nilipoenda kutembelea gerezani, wafungwa 30 waliofungwa maisha kwa kesi za kufanya ukatili. Pia takwimu za ubakaji, ulawiti na ukatilili wa kingono kuanzia Januari hadi Novemba, 2019 kesi zilizojulikana ni watoto 404 na wanawake 37 ambao wamefanyiwa ukatili. Jambo hii la ukatili linasababisha ongezeko la maambukizi ya UKIMWI, kwani Mkoa upo katika nafasi ya 11.3% na 43% ya udumavu hivyo bado tuna kazi kubwa ya kupambana vita hivi. Tatizo hili linachangiwa na mambo ya mila na desturi, Ushirikina, ulevi wa kupindukia.

Mwisho Mheshimiwa Hapi amesisitiza kuwa, jamii na wadau itoe macho katika maeneo ya kuonesha sinema, kwenye masomo ya ziada (tuition), waganga wa jadi ili ijulikane nini kinaendelea katika maeneo hayo.


Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.