• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Ally Hapi awakutanisha Wadau wa Chai na Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi katika kutatua mgogoro wa ulipaji ushuru Wilayani humo tarehe 12/12/2019

Posted on: December 12th, 2019

Akitoa ufafanuzi katika mgogoro huo Mkurugenzi wa Halmashari ya Wilaya ya Mufindi Ndugu Netho Ndilito amesema, baada ya kufanya tathimini tuliwaita mara kadhaa kwa barua wadau hawa wa chai ili waje tuzungumze mezani na tukubaliane lakini hawakutaka kuja. Sisi kama Halmashauri tuliamua kuwapeleka Mahakamani. Lakini kabla ya kwenda huko tukaomba Mkuu wa Mkoa atukutanishe na tupate suruhu ya jambo hilli.

Katika kufafanua zaidi chanzo cha mgogoro huo Msaidizi wa Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Ndugu Method Msokele amesema, tuliona tathmini yetu kuwa hakuna malipo ya ushuru kutoka kwa Wadau wa Chai na kwamba Kampuni hizi za Chai hazijawahi kulipa ushuru wa chai wa kiasi cha 3% wa mapato yao ya chai. Kwa mujibu wa sheria kifungu VII (b) wadau wanatakiwa kulipa ushuru kwa Halmashauri, kwani imeonesha kuwa Kampuni ya Uniliver inadaiwa zaidi ya Bilioni 82, Mufindi Tea Company (MTC) inadaiwa zaidi ya Bilioni 30 na Kampuni ya Kiganga (Kisigo Factory) inadaiwa zaidi ya Milioni 993 za Kitanzania.

Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mheshimiwa Jamhuri David amesema, sisi na wawekezaji tunafanya kazi kwa ukaribu sana kwani wameajiri watu wengi ambao wanajipatia kipato. Linapojitokeza tatizo kama hili huwa tunachukulia uzito sana, sasa kwa vile leo Mkuu wetu wa Mkoa upo hapa umetukutanisha nadhani jambo hili litafikia muafaka.

Mkuu wa Idara ya Fedha kutoka Uniliver Ndugu Rayson Raja amekiri kuwa na mvutano kati yao, hivyo ameomba wakubaliane na Halmashauri na kuondoka katika mgogoro huo.

Meneja wa MTC Ndugu Mohamed Kasila naye amekiri kuwa na mvutano huo na kuomba kupitia meza ya makubaliano kufikia muafaka wa jambo hili. Kwani fedha wanazodaiwa ni nyingi mno hawataweza kuzilipa.

Mwakilishi wa Bodi ya Chai Ndugu Junis Mwano amesema ukumu la Bodi ya Chai ni kutunza kumbukumbu za kila Kampuni na tunazichakata kila mwezi. Pia amesema Halmashauri zina uwezo wa kutengeneza sheria ndogo za ulipaji ushuru na ipelekwe kwa Wadau ili wazipitie kabla hazijaanza kutumika.

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa baada ya kusikiliza pande zote mbili kwa utulivu kabisa alimaliza kwa kusema, mimi kama Mkuu wa Mkoa kazi yangu kubwa ni kusimamia Sheira na Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika pande zote mbili kuna hoja ambazo zinakinzana. Hivyo basi nalazimika kuunda kamati ndogo maalum ambayo itakaa mezani wachakate taarifa zote ili tupate ukweli wa jambo hili. Sitapenda kusikia kuwa pande Fulani imekataa kukaa na kuzungumza, naomba mzungumze kwa kufuata sheria na taratibu bila upendeleo wala mahaba wala chuki. Nitatoa muda maalumu wa kamati hii kushughulikia jambo hili, baada ya hapo nitakaa na kamati yangu kushauriana nini kifanyike.

Rai yangu ni kuwa nidhamu ya kukutana na heshima iwepo, kila kampuni itajua waoe watu gani (wataalamu), kwa sababu wote tunatambua umuhimu wa Sekta ya chai. Pia Bodi ya Chai lazima muwepo katika mazungumzo haya.

Nawapongeza Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi kwa na nia ya kukusanya mapato, pia Sekta Chai kuonesha nia ya kufanya mazungumzo haya ili tufikie muafaka.

Imetolewa na Ofisi ya Habari,

Mkoa wa Iringa,

Humphrey Kisika. 

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.