• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

MOTO WA IRINGA MPYA KUUNGUZA WATUMISHI WAZEMBE

Posted on: September 11th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa-Iringa

Moto wa Iringa mpya kuunguza watumishi wa Serikali wazembe na wanaoingia ofisini muda wanaotaka mkoani Iringa.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi wa Tarafa ya Kibengu katika siku ya tatu ya ziara yake ya Tarafa kwa Tarafa mkoani Iringa leo.

Mhe Hapi alisema kuwa kutokana na utendaji kazi wa mazoea, wapo baadhi ya watumishi wanaoingia ofisini muda wanaotaka wao. “Moto wa Iringa mpya utakwenda kuwaunguza watendaji hao wote. Bahati nzuri mimi siyo mtu wa kukaa ofisini, nimeamua kuzunguka Tarafa zote 15 za Mkoa wa Iringa ili kuwasha moto huu. Hakika hautamuacha mtumishi wa aina hiyo salama”. Serikali ya Mhe Dkt John Pombe Magufuli imetoa fedha nyingi kuwaletea maendeleo wananchi, wapo watumishi wamegeuka mchwa, wanaotafuna fedha za miradi ya maendeleo ya wananchi. “Nimekuja mwenyewe kukagua miradi hiyo. Nataka niwahakikishie ndugu zangu wananchi kuwa watumishi wa aina hiyo hawatabaki salama” alisisitiza Mhe Hapi.

Katika kuhakikisha watumishi wa Serikali wanafanya kazi, aliagiza kuwa kila mtumishi wa Serikali kutoa taarifa ya kila wiki ya utekelezaji wa majukumu yake ya kazi. “Taarifa hizo zitakuwa za aina mbili. Aina ya kwanza ni kazi alizofanya wiki iliyopita na aina ya pili ni kazi atakazotekeleza wiki ijayo” alisema Mhe Hapi.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa yupo katika siku yake ya tatu ya ziara ya Tarafa kwa Tarafa akiwa katika Tarafa ya Kibengu amezindua nyumba moja ya walimu ya familia sita katika shule ya sekondari Ilogombe, kukagua ujenzi wa bweni la wanafunzi na miundombinu ya shule ya sekondari Kihansi na kufanya mkutano na wananchi wa Tarafa ya Kibengu.

=30=

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.