• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RC ALLY HAPI AWASHUKIA MAKAMPUNI YANAYOKWEPA KULIPA KODI

Posted on: January 10th, 2019

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, IRINGA

Mkuu wa mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi amezitaka kampuni zote zilizopo mkoani Iringa zinazojishughulisha na ununuzi na uuzaji wa mbao pamoja na uuzaji wa nguzo za umeme kuhakikisha wanalipa kodi ya asilimia tano(5%) kwa mujibu wa sheria za nchi hii.

Ameyazungumza hayo hii leo wakati wa kikao cha wadau mbalimbali alipokuwa akiwasilisha maagizo yaliyotoka kwa waziri mkuu wa serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Kasimu Majaliwa kwenye kikao kilichofanyika jijini Dodoma baada ya kutokea sintofahamu juu ya tatizo la nguzo za umeme.

“Jamani vita ya kupambana na wafanyabiashara wanaokwepa kodi sio jambo rahisi kama ambavyo mnavyofikiri ni vita kubwa kweli kweli na inatisha haswa,hivyo hadi kuona hii leo nimeshinda ujue kuwa serikali ya awamu ya tano haitaki mchezo mchezo kwenye mapato ambayo yanatakiwa kulipwa kwa mujibu wa sheria” alisema Hapi

Wananchi wengi wa Iringa ni maskini wakati wanadhahabu kubwa ya maliasili ya misitu ambayo ndio tegemeo la watanzania kwa asilimia tisini(90) kwa kuwa zao la mbao na nguzo zote zinatoka mkoani Iringa hivyo ni lazima walipe kodi ya asilimia tano ili kuboresha na kuwaondoa wananchi wa mkoa wa iringa kwenye umaskini.

“Hakuna sheria ya kulipa elfu tano kwa nguzo za umeme na mbao bali kuna sheria ya 5% ya kodi ambayo kila mfanyabiashara wa nguzo za umeme anatakiwa kulipa, Hivyo natangaza kuanzia leo wafanyabiashara wote wanatakiwa kulipa hiyo 5% ya kodi ya nguzo za umeme na mbao” alisema Mhe. Hapi

Vilevile mkuu wa mkoa amewaagiza wakurugenzi wote kuhakiki tozo zote za makampuni yanayofanya biashara ya mbao na nguzo za umeme ili kupata mapato yatakayosaidia kuboresha sekta ya Elimu, Afya na kuboresha miundombinu ya wananchi ambao wanachangia kodi kwa maendeleo ya nchi yao.

Serikali ya mkoa wa Iringa haitawavumilia wafanyabiashara wowote wale ambao wanakwepa kodi kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi nitawachukulia hatua kali kweli kweli kwa kuwa serikali ya awamu ya tano imewahamasisha wananchi kulipa kodi na wanalipa sasa iweje makampuni ndio yanakwepa kulipa kodi? kwa mkoa huu haitawezekana.

Nawaomba wawekezaji wazawa wa viwanda vya kuchakata mbao na nguzo za umeme kuja kuwekeza mkoani Iringa kwa kuwa bado kuna fursa hiyo na mkoa utahakikisha wawekezaji wazawa wenye sifa wanapata fursa hiyo hata kuiuzia serikali mazao hayo ya mbao na nguzo za umeme.

“Tukiwa na wawekeazji wazawa nina uhakika hawawezi kukwepa kodi maana hakuna sehemu ya kukimbia kwa kuwa hii nchi ni yao lakini pia itachangia ushindani katika soko na kuacha kuitegemea kampuni moja tu ambayo inakwepa kulipa kodi” alisema hayo mkuu wa mkoa Mhe.Hapi.

Mkuu wa mkoa wa Iringa ameitaka kampuni ya uzalishaji na uuzaji wa nguzo za umeme ya New forest, kulipa hilo deni kwa Halmashauri ya Kilolo kiasi cha bilioni 2,970,664,213.82. Pia amezitaka Halmashauri za Mafinga Mji na Mufindi dc kuandaa bili za madai hayo na kisha kuwasilisha kwa kampuni zilizopo katika Halmashauri hizo kwa ajili ya ulipaji wa tozo hizo.

Hata hivyo Mhe. Hapi alisema kuwa kampuni hiyo ya New forest imekuwa ikikwepa kodi tangu mwaka 2007 ilipoanzishwa mpaka sasa ni miaka 12 imekuwa ikisema bado hawajaanza kupata faida kitu ambacho sio kweli. Hivyo amewaagiza TRA na vyombo vya usalama kukagua mali zao zote ili kujua kama kweli hawapati faida.


Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.