• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RC HAPI AKATAA KUWEKA JIWE LA MSINGI KLINIKI YA UZAZI NA AFYA YA MTOTO MUFINDI

Posted on: September 9th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi amekataa kuweka jiwe la msingi jengo la kliniki ya uzazi na afya ya mtoto katika kituo cha afya Mgololo, wilayani Mufindi  baada ya kutoridhishwa na gharama kubwa za ujenzi zilizotumika.

Akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya Tarafa kwa Tarafa ya kutembelea Tarafa 15 za Mkoa wa Iringa, iliyoanzia katika Tarafa ya Kasanga Wilaya ya Mufindi, alipangiwa kutembelea na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la kliniki ya uzazi na afya ya mtoto. Mhe Hapi alikataa kuweka jiwe la msingi baada ya kukagua ujenzi wa jengo hilo lililogharimu kiasi cha shilingi milioni 360. “Siwezi kuweka jiwe la msingi katika jengo hili. Nataka kujiridhisha na thamani ya fedha katika mradi huu. Mnapotengeneza makadirio ya gharama za ujenzi wa mradi (BOQ) makubwa mnamkatisha tamaa muwekezaji. Nataka maelezo kutoka Wakala wa ujenzi Tanzania (TBA) nani kaandaa makadirio ya gharama za ujenzi wa mradi huu” alihoji Mhe Hapi. Maeneo mengi tumejenga Zahanati kwa gharama za shilingi milioni 400, iweje jengo hili tu la kliniki ya uzazi na afya ya mtoto ligharimu shilingi milioni 360, aliendelea kuhoji, Mhe Hapi.

Akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa jengo la kliniki ya uzazi na afya ya mtoto, katika kituo cha afya Mgololo kwa Mkuu wa Mkoa, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Dkt Fredrick Mugarula alisema kuwa ili kukamilisha ujenzi wa jengo la kliniki hiyo, imekadiriwa kutumia kiasi cha shilingi milioni 360. “Serikali kupitia ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa na TBA wameweza kutoa marekebisho ya ramani na makisio ya ujenzi” alisema Dkt Mugarula.

Akiongelea matarajio ya mradi huo, alisema kuwa baada ya ujenzi kukamilika, Halmashauri inatarajia kuwa na ongezeko kubwa la wateja katika kliniki hiyo kutokana na mazingira yenye kutoa huduma bora. Aidha, hali hiyo itapunguza vifo vya kina mama na watoto vilivyokuwa na uhusiano wa kutopata huduma bora za afya.

Kituo cha afya Mgololo ni miongoni mwa vituo tisa vya afya vinavyotoa huduma katika Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, kikiwa kilianzishwa mwaka 1985 na Baba wa Taifa Mwl Julius Nyerere kama sehemu ya kiwanda cha karatasi Mgololo.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.