• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RC - QUEEN "SITAKUJA KUFANYA ZIARA ZA KUSHITUKIZA"

Posted on: June 1st, 2021

RC - QUEEN "SITAKUJA KUFANYA ZIARA ZA KUSHITUKIZA"

MKUU Wa Mkoa Wa Iringa Queen Sendiga, amewataka watumishi wa sekta ya afya kufanya kazi kwa uadirifu bila kushurutishwa, huku akisema katika uongozi wake hatakuja kufanya ziara za kushitukiza bali atataka kila mfanyakazi wa umma kujua wajibu wake akiwa mahala pake pa kazi

Hayo aliyasema jana wakati wa ziara ya kukagua ufanisi wa kazi katika hospitali ya rufaa ya mkoa

Alisema endapo kila mmoja atajua wajibu na majukumu yake hakuna haja ya kushitukizana ,na ndio maana alienda akiwa ametoa taarifa kwamba anaenda ila itakapo bidi atafanya hivyo

"Mnaweza mkajiuliza mbona mkuu huyu hatumii ziara za kushitukiza kama wengine ambao wakifika wanakimbizana kwenye habari ya kufanya ziara kwa kushitukiza, niseme tu sisi wote ni watumishi wa umma ile habari ya kwenda mahali na kuaza kukurupushana kwangu naona kama haina tija ,"alisema Mkuu wa mkoa

Aidha alimuagiza mganga mkuu kuwashughurikia wahudumu wote ambao hawatoi huduma ipasavyo kukaa nao na kuwaambia wajirekebishe na kama hawawezi wanaona taaruma waliyoisomea hawakujua itakuwa na majukumu makubwa waache wakafanye kazi nyingine

Pia aliwaomba watumishi wote wawe na maadili katika kazi zao kwani hatakuwa tayari kupokea malalamiko ya aina yoyote yale kutoka kwa wananchi kuhusu utendaji kazi wa wahudumu

"Najua kwamba kuna, upungufu wawauguzi lakini isiwe sababu ya kushidwa kufanya kazi kwani ndio kazi tuliyopewa tuifanye kwa moyo wote, alisema Queen.

Queen alisema matarajio na mategemeo yake makubwa ni kuziboresha huduma za afya ili kuwasaidia wananchi.

Aidha amesema anajua kuwa sekta ya afya inachangamoto na tayari amekaa na viongozi wamemueleza mambo yote na anafanya kila namna kuhakikisha anazishughulikia

"Hivi karibuni nategemea kwenda Dodoma nitahakikisha nakutana na viongozi wa sekta husika ya wizara ya afya ili kuona wanatusaidiaje hata kwa hela kidogo tuliyonayo tuweze kupatiwa mahitaji yetu" alisema Aliendelea kusema, nimesikia tatizo la upungufu ya wataalamu bingwa wa magonjwa mbalimbali hivyo nitaongea na waganga wa mkoa ili waorodheshe changamoto zote ili zikitoka fursa za ajira tuone na sisi wanatusaidiaje ,"alisema Queen

Pia alisema ameridhishwa na utoaji huduma wa hospitali hiyo pamoja na watendaji wake namna wanavyo wajibika licha ya hayo pia alisema kumekuwa na baadhi ya wahudumu kutumia lugha chafu kwa wagonjwa na kuwataka kuacha maramoja kwani kazi hiyo ni wito kama zilivo kazi nyingine

Alisema maadili ya wauguzi ni tofauti na maadili ya kazi nyingine hivyo kashifa, chuki, majibu yasiyoridhisha na vikwanzo vya aina yeyote havitakiwi kwa wauguzi

"Ningumu kumtambua mtu mwenye tabia hizo kwasababu ya wingi wenu hivyo lazima ujichunge mwenyewe na kwakuwa kuna viongozi tutazidi kukumbushana,"alisema

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.