• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

RC: SERUKAMBA AMEWAAGIZA WASIMAMIZI WA MIRADI YA UJENZI KUONGEZA MAFUNDI

Posted on: April 24th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba amewaagiza wanaosimama ujenzi wa miradi kuhakikisha wanaongeza mafundi wa kujenga katika miradi hiyo ili kukamilisha miradi kwa wakati.

Ameyasema hayo leo wakati aKifanya ziara ya kukagua miradi katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ambapo ametembelea katika shule ya msingi Kiwere, Shule ya Sekondari Kiwere, Shule ya msingi Itagutwa, shule ya Sekondari Furahisha na shule ya Sekondari ya Ismani ambapo amekagua na kuwataka wasimamizi wa maradi hiyo kumaliza miradi kwa wakati

Akiwa katika shule ya msingi ya Kiwere ambapo kuna mradi wa ujenzi wa vyoo amempa wiki tatu msimamizi wa jengo hilo kwanza kuhakikisha anaongeza mafundi na kukamilisha ujenzi wa vyoo hivyo kwa wakati nakama atashindwa basi kazi atapewa mtu mwingine ambaye atamaliza mradi huo kwa wakati.

Pia akiwa katika shule ya Msingi Itagutwa ambayo ina mradi wa ujenzi wa madarasa mawili na Ofisi moja unaogharimu kiasi cha Shilingi Million 40 amemtaka msimamizi wa jengo hilo kukamilisha mradi kwa wakati ili Watoto waanze kuyatumia madarasa hayo.

Nao baadhi ya wazazi na wananchi kutoka katika kata ya Itagutwa wameishukuru Serikali kwa ujenzi wa majengo hayo ambapo wamesema kutokana na madarasa yaliyopo kuwa ni mabovu basi madarasa hayo mapya yatakuwa mkombozi kwa wanafunzi hao.

Sambamba na hayo Mhe. Serukamba amepongeza kasi ya ujenzi wa madarasa na vyoo inayoendelea katika shule ya sekondari Kiwere, Ismani na Shule ya Sekondari ya Furaha

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.