• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Serikali kutatua kero za Wafanyakazi- Dkt Magufuli

Posted on: May 1st, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Serikali ya awamu ya tano itaendelea kushughulikia kero za wafanyakazi na kuboresha maslahi ili wafanye kazi kwa kujituma na tija zaidi.

Kauli hiyo ilitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli alipokuwa akihutubia mamia ya wafanyakazi waliofurika katika uwanja wa michezo wa Samora mjini Iringa katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani.

Dkt Magufuli alisema kuwa serikali yake itaendelea kushughulikia kero na kuboresha maslahi ya wafanyakazi nchini. “Leo ni siku ya wafanyakazi, napenda kutumia fursa hii kuwapongeza wafanyakazi kwa mchango wenu mkubwa wa kuiletea nchi maendeleo. Hongereni sana”. Aidha, aliwataka watumishi hao kutanguliza nidhamu na uwajibikaji katika utendaji wao wa kazi. “Mtumishi akiwa mvivu na mzembe anakuwa ni mnyonyaji” alisema Dkt. Magufuli.

Kuhusu wafanyakazi kuhamishwa bila kulipwa stahili zao, Rais Dkt Magufuli alimuagiza waziri mkuu kuwasimamia wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa ambao bado wanahamisha wafanyakazi bila kuwalipa stahili zao. “Waziri mkuu nakuomba ulisimamie hilo. Hatuwezi kuwa tunatoa maagizo halafu mtu mwingine aendelee kufanya hivyo. Tulishatoa maagizo mtu asihamishwe bila kulipwa. Naagiza tena viongozi ndani ya serikali wasihamishe bila kulipa fedha za uhamisho. Ni matumaini yangu sitarudia tena kuzungumzia hili katika maisha yangu”.

Akiongelea malimbikizo ya watumishi, alisema kuwa serikali yake imelipa malimbikizo kwa watu 52,852 yenye thamani ya shilingi bilioni 86,323. Vilevile, aliwahakikishia watumishi kuwa wale wote wenye madai halali watalipwa haki zao. “Kwa hizi nyuso za furaha mnazonionesha leo, ningekuwa na hela kwenye chungu zimebaki pale, leo ningetamka tu. Lakini nikitamka ntazitoa wapi? Nina mpango wa kuajiri wafanyakazi 52,000 ntawalipa nini? Dhamira yangu inanituma kwamba kusubiri ni kitu kizuri. Hebu tujenge miundombinu na kuajiri hawa 52,000. Tutaendelea kulipa viporo vya madeni hadi viishe” alisema Dkt Magufuli.

=30=

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.