• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

Serikali ya awamu ya sita ya Rais Samia Suluhu Hassan imesikia kilio cha wananchi wa kata ya Udekwa wilayani Kilolo mkoani Iringa

Posted on: January 18th, 2022

WALIOKUWA WAKITUMIA BARABARA YA KM 60 WAPATA YA KM 20

SERIKALI ya awamu ya sita ya Rais Samia Suluhu Hassan imesikia kilio cha wananchi wa kata ya Udekwa wilayani Kilolo mkoani Iringa ambao kwa miaka mingi waliomba bila mafanikio kujengewa barabara inayounganisha kijiji chao na cha Mahenge.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Queen Sendiga alisema ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa Kilometa 20 utawanufaisha wananchi wa kijiji hicho kusafiri na kusafirisha bidhaa zao kwa urahisi kwenda kijiji cha Mahenge kilichopo barabara kuu ya Iringa, Dar es Salaam.

Alisema kwa miaka yote wananchi wa  kata hiyo wamekuwa wakilazimika kusafiri kwa kupitia barabara ya Udekwa, Ilula yenye urefu wa zaidi ya kilometa 60 ili kufika katika kijiji cha Mahenge

Mkuu wa Mkoa alitoa taarifa hiyo juzi kwa Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa inayotembelea halmashauri zote za mkoa wa Iringa kukagua utekelezaji wa Ilani na ahadi za maendeleo zilizotolewa na chama hicho kwa wananchi..

“Tunaipongeza serikali ya awamu ya sita, hakika imesikia kilio cha wananchi wanyonge wa Udekwa. Badala ya kusafiri kwa zaidi ya kilometa 60 kufika Mahenge, sasa tutasafiri kilometa 20 tu. Ujenzi wa barabara hii umetupunguzia umbali wa safari kwa zaidi ya kilometa 40,” alisema mkazi wa kijiji hicho, Adriano Mahenge.

Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tarura)) wa wilaya ya Kilolo, Mhandisi Nkanda Kidola alisema mpaka sasa ujenzi wa barabara hiyo unaendelea vizuri ukiwa umefikia asilimia 70 ya ujenzi wake .

Mhandisi Kidola alisema hadi kukamilika kwake barabara hiyo inayojengwa kwa kiwango cha changarawe kwa kupitia fedha za tozo ya mafuta, itagharimu Sh Milioni 500.

“Barabara hii pia inaweza kutumika kama njia ya mchepuko endapo barabara ya Mahenge, Kitonga hadi Ilula itakuwa na dharula. Magari yanayokwenda Dar es Salaam na Iringa Mjini yanaweza kutumia barabara hii kuepuka dharula hiyo na kuendelea na safari,” alisema.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Dk Abel Nyamahanga ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati hiyo ya siasa alimpongeza Rais akisema ahadi zake za kutumia tozo mbalimbali zilizobuniwa na serikali kutekeleza miradi mbalimbali zimeanza kuleta tija.

“Ni jambo la kujivunia sana kuona barabara hii iliyoshindikana kujengwa kwa miaka mingi na moja ya sababu yake ikiwa ni ufinyu wa bajeti, sasa inajengwa tena kwa fedha zetu wenyewe,” alisema.

Mbunge wa Jimbo la Kilolo, Justin Nyamoga, aliishukuru serikali kwa kutatua changamoto ya barabara hiyo akisema itachochea zaidi shughuli za kiuchumi zinazofanywa na wananchi wa Udekwa na wilaya ya Kilolo kwa ujumla wake.

Alisema sehemu kubwa ya kata ya Udekwa inapitiwa na hifadhi ya Taifa ya Udzungwa na hifadhi ya mazingira ya asili Kilombero hivyo kujengwa kwa barabara hiyo kutawavutia watalii wengi na hatimaye kukuza pato la wananchi, kata, wilaya, mkoa na Taifa kwa ujumla.

Pamoja na kukagua ujenzi wa barabara hiyo, kamati hiyo ya siasa imetembelea miradi ya madarasa yaliyojengwa kwa fedha za mkopo uliotolewa na Shirika la Fedha Duniani (IMF) hivikaribuni, kituo cha afya Ilula na miundombinu ya maji Image.






Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.