• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

UTALII KUSINI UNAKABILIWA NA TATIZO LA MIUNDOMBINU

Posted on: February 12th, 2018

Na. Dennis Gondwe, Iringa

Kanda ya kusini inakabiliwa na changamoto ya miundombinu inayosababisha vivutio vingi vya utalii kutofikika kirahisi na watalii kukosa fursa ya kuona hazina hiyo.

Kauli hiyo imetolewa na makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan katika hotuba yake wakati wa uzinduzi wa mradi wa kuimarisha usimamizi wa maliasili na kuendeleza utalii kanda ya kusini mwa Tanzania (REGROW), uzinduzi uliofanyika eneo la Kihesa Kilolo mjini Iringa leo.

Hassan alisema kuwa ukanda wa kusini una vivutio vingi vya utalii ambavyo havifahamiki na kufikika. “Kama mnavyofahamu, kuwa ukanda huu una vivutio vingi vya utalii ila kutokana na changamoto za miundombinu, vivutio hivi havifikiki. Katika ziara yangu mkoani hapa nimeshuhudia changamoto ya miundombinu ya barabara katika baadhi ya maeneo, ila napenda kuwahakikishia kuwa serikali ina dhamira ya dhati ya kuleta mabadiliko katika sekta hii kwa kuhakikisha kuwa tunatanua mtandao wa barabara na pia kuweka mikakati thabiti ya kuendeleza vivutio vya utalii vilivyoko kanda ya kusini ili vichangie kwa ukamilifu ukuaji wa uchumi na ustawi wa wananchi” alisema Hassan. Aliongeza kuwa kanda ya kusini imejaaliwa hifadhi ya taifa ya Ruaha, Kitulo, milima ya Udzungwa na pori la akiba la Selous. Mengine ni hifadhi ya misitu ya asilia ya Kilombero, milima Rungwe na mashamba ya miti na maliasili.

“Vivutio vya utalii kanda ya kusini vinajumuisha maeneo ya kihistoria ya Kalenga na isimila (Iringa), kumbukumbu za vita vya Majimaji (Ruvuma), Kimondo cha Mbozi (Songwe) maporomoko ya Kalambo (Rukwa), ziwa Ngozi (Mbeya), fukwe nzuri zilizoko katika ziwa Nyasa, Mtwara na Lindi” alisema Makamu wa Rais. Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kutumia fursa hizo kukuza sekta ya utalii.

Akimkaribisha makamu wa Rais, waziri wa maliasili na utalii, Dr. Hamis Kigwangala alisema kuwa mradi wa kuimarisha usimamizi wa maliasili na kuendeleza utalii kanda ya kusini mwa Tanzania (REGROW), utaboresha miundombinu hafifu ya barabara kwa ajili ya kuyafanya maeneo ya vivutio kufikika kirahisi na kuchochea utalii. Aidha, elimu kwa umma itapewa kipaombele katika etekelezaji wa mradi huo.

Kuhusu mapambano dhidi ya ujangili, waziri wa maliasili na utalii, aliwataka wale wote wanaojihuisisha na ujangili kutafuta kazi nyingine ya kufanya. “Wizara tumejiwekea mkakati wa kupambana na ujangili kufikia asilimia sifuri. Wito kwa majangili watafute kazi nyingine ya kufanya. Tutapambana nao kulia na kushoto, mbele na nyuma mpaka tuwamalize” alisema Dr. Kigwangala.

Katika salamu za mkuu wa mkoa wa Iringa, amina masenza alisema kuwa mkoa wa iringa ulichaguliwa kuwa kitovu cha utalii kwa ukanda wa kusini na wizara ya maliasili na utalii kwa lengo la kukuza sekta hiyo kanda ya kusini. Katika kuhakikisha sekta ya utalii inakuwa, mkoa huo umeunda kamati ya utalii na mikoa mingine kufanya hivyo alisema. Aliongeza kuwa utalii ni agenda ya kudumu mkoani hapo.

Mradi wa kuimarisha usimamizi wa maliasili na kuendeleza utalii kanda ya kusini mwa Tanzania (REGROW) unalenga kukuza utalii na kipato cha wananchi kwa kuboresha miundombinu, kujenga uwezo katika usimamizi wa maliasili na kuwezesha wananchi wanaozUnguka hifadhi kuzalisha kwa tija.

=30=

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.