• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

WAKURUGENZI MUFINDI WATAKIWA KUSIMAMIA MIRADI

Posted on: September 15th, 2018

Na. Dennis Gondwe, Afisa Habari, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa- Iringa

Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wilayani Mufindi wametakiwa kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili iendane na thamani ya fedha zinazotolewa na Serikali.

Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi alipokuwa akifanya majumuisho ya ziara yake ya Tarafa kwa Tarafa wilayani Mufindi katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi jana.

Mhe Hapi alisema “wakurugenzi simamieni vizuri utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yenu ili kujiridhisha na thamani ya fedha iliyotumika katika utekelezaji wake. Kuna madudu mengi yanafanyika katika miradi ya maendeleo kutokana na watumishi wasio wazalendo”. Vilevile, aliwataka watumishi wa umma na taasisi binafsi kusimamia miradi iliyokusudiwa kutekelezwa kwa kuzingatia falsafa ya Iringa mpya, ili iwe na viwango na maslahi kwa Taifa.

Aidha, aliwataka kusimamia watumishi wanaowaongoza ili wawahudumie wananchi vizuri. “Katika Iringa mpya nataka wananchi wetu wahudumiwe vizuri hasa wananchi wanyonge. Wananchi wanyonge hawana fedha za kwenda mahakamani, wananchi wanyonge hawana fedha za kwenda kwenye mabaraza ya Ardhi wala hawana nauli ya kusafiri kwenda kufuatilia haki zao. Tukiwakwaza hawa hawana mtu wa kumlilia wala kushtaki zaidi ya kusubiri viongozi wawatembelee” alisisitiza Mhe Hapi.

Akiwa wilayani Mufindi, Mkuu wa Mkoa alitembelea Tarafa za Kibengu, Kasanga, Sadani, Malangali na Ifwagi. Pamoja na mambo mengine, alifanya mikutano mikubwa mitano ukiwemo mkutano wa uzinduzi wa kampeni ya Iringa mpya na mikutano midogo midogo 12 na wananchi kupewa fursa ya kuhoji na wataalam kujibu kero za wananchi.

=30=

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.