• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

WANANCHI WA MIKOA YA IRINGA, TANGA, LINDI NA GEITA WANATARAJIA KUNUFAIKA NA MRADI WA UBORESHAJI WA BARABARA VIJIJINI

Posted on: June 20th, 2023

WANANCHI katika Mikoa ya Iringa, Tanga, Lindi na Geita wanatarajia kunufaika na Mradi wa Uboreshaji wa Barabara Vijijini kwa Ushirikishwaji wa Jamii na Ufunguaji wa fursa za kijamii na kiuchumi (RISE), ambapo zaidi ya shilingi bilioni 822  zitatumika kuboresha miundombinu ya barabara vijijini.

Mhe, halima Dendego Mkuu wa Mkoa Iringa amesema kuwa kusaini Kwa mikataba hii ni faraja kubwa Kwa wananchi wake kwani kilikuwa ni kilio cha muda mrefu sana Kwa sababu ujenzi wa barabara hizo zitakuza uchumi wa wananchi wangu na pia mazao kufika Kwa wakati sokoni na viwandani, tofauti na sasa hususani kipindi cha mvua magari mengi yanakwama na kukaa muda mrefu na kusababisha wakulima kupata hasara kubwa.

Hata hivyo amewataka wananchi kushirikiana na wakandarasi hao na amewaonya wale wasio waaminifu hata chukua hatua Kali dhidi yao.

Akizungumza katika hafla ya utiaji saini mikataba ya ujenzi na usimamizi baina ya TARURA na wakandarasi wa ujenzi na usimamizi wa mradi wa RISE iliyofanyika Mkoani Iringa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Angela Kairuki (Mb), amesema, mradi huo wa RISE unaenda kuwakomboa wananchi hasa waishio vijijini kwa kuwafungulia fursa za kijamii na kiuchumi.

Amesema Serikali ya Awamu ya Sita kupitia TARURA imekuwa ikifanya jitihada za dhati kuhakikisha kuwa inaboresha barabara za vijijini ili ziweze kupitika muda wote wa mwaka na ndiyo maana tangu Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, aingie madarakani Bajeti ya TARURA imeongezeka kwa takribani mara tatu kutoka bilioni 200 mwaka 2021 hadi bilioni 836 kwa mwaka 2023/2024.

Aidha, amemshukuru Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwajali watanzania wa hali ya chini na kueleza kuwa hawana cha kumlipa bali waendelee kumuunga mkono kwa hali na mali aendelee kuwatumikia.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa TARURA, Mhandisi Victor Seff, amesema kuwa lengo la mradi wa (RISE) ni kuboresha barabara za vijijini, kutoa fursa za ajira kwa wananchi katika maeneo ya vijijini yaliyochaguliwa na kujenga uwezo wa kitaasisi katika usimamizi endelevu wa barabara za vijijini kwa kutumia mbinu za ushirikishwaji wa jamii.

Imetolewa na Afisa Habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.