• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

WATUMISHI WA MAHAKAMA MSITOE WALA KUPOKEA RUSHWA - RC SERUKAMBA

Posted on: February 3rd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba amewasisitiza Watumishi wa mahakama nchini kuwa waadilifu na kuepuka rushwa kwani ni kikwazo katika kujenga Taifa bora.Ameyasema hayo  Februari 03, 2025 wakati wa maadhimisho ya kilele cha siku ya sheria yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Mahakama Kuu ya Tanzania Mkoani Iringa.Mhe. Serukamba amesema kuwa wanasheria wanapaswa kupambana na Rushwa kwani ni Adui wa haki kwa kuwa watu wengi wanakosa haki zao kwa Sababu ya Rushwa.Aidha Mhe. Serukamba ameongeza kuwa wanapoongelea Dira ya 2050 wanapaswa kujenga jamii iliyo bora yenye haki,usawa na wasitoe wala kupokea rushwa ili pawepo na taifa lenye maendeleo.Pia Mhe. Serukamba ameeleza na kuomba kuwa kila mwananchi anapaswa kuwa na elimu ya sheria ili kuepuka migogoro na kufanya jamii kuwa na amani na utulivu ili kuwa na Taifa endelevu na lenye maendeleo katika nyanja tofauti tofauti.Naye Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu Kanda ya Iringa, Dunstan Ndunguru wakati akisoma taarifa inayohusu maadhimisho hayo amefafanua kwamba mahakama katika kipindi cha wiki hiyo imefanikiwa kufanya maonyesho ya huduma zinazotolewa na mfumo wa haki za kisheria na namna wananchi wanavyoweza kutumia huduma hizo ili kulinda haki zao. Akiendelea kuzungumzia maadhimisho hayo Ndunguru amesema kuwa maonyesho hayo yalijumuisha utoaji wa elimu kuhusu sheria za familia, urithi, kazi, na haki za watoto, ikiwa ni njia mojawapo ya kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuwaelimisha kuhusu masuala ya kisheria.Ikumbukwe kuwa  maadhimisho hayo ya wiki ya sheria yalianza mkoani Iringa Januari 25 mpaka Februari mosi mwaka huu na kilele chake kikiwa ni leo Februari 03, 2025 huku Kauli mbiu  ikiwa ni "Tanzania 2050 Nafasi ya Taasisi zinazosimamia Haki, Madai katika kufikia Malengo makuu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo".

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.