• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

DK MAHIGA AZIKARIBISHA NCHI JIRANI MAONESHO YA UTALII YA KARIBU KUSINI

Posted on: October 3rd, 2017

DK MAHIGA AZIKARIBISHA NCHI JIRANI MAONESHO YA UTALII YA KARIBU KUSINI

Na. Frank Leonard

WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Augustine Mahiga amezikaribisha nchi jirani za Zambia, Malawi, Msumbuji na Kongo kushiriki maonesho ya Utalii ya Karibu Kusini yatakayokuwa yakifanyika kila mwaka mjini Iringa baada ya serikali kuutangza mkoa wa Iringa kuwa kitovu cha utalii cha mikoa ya Nyanda za Juu Kusini.


Aliyasema hayo jana wakati akifunga maonesho ya mwaka huu yaliyofanyika katika viwanja vya Kichangani mjini Iringa kati ya Septemba 29 na Oktoba 2.


“Ni maonesho yanayohusisha mikoa saba ya Nyanda za Juu Kusini ya Iringa, Njombe, Ruvuma, Mbeya, Songwe, Rukwa na Katavi. Muda umefika sasa tuzishirikishe nchi jirani na mikoa hii ili kuyafanya maonesho haya yawe ya kimataifa zaidi,” alisema.


Pamoja na kuzialika nchi hizo jirani, ameahidi kusambaza taarifa maalumu ya vivutio vya utalii vya kusini kwa mawakala mbalimbali wanaotangaza utalii wa Tanzania nje ya nchi.


Akifunga maonesho hayo Balozi Mahiga alisema; “Nimefurahishwa sana kushirikishwa katika maonesho hayo natarajia mwakani nitakuwa pamoja nanyi.”


Awali Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alitoa takwimu zinazoonesha maonesho hayo yaliyofanyika kwa mara ya kwanza mwaka jana yakipata mafanikio zaidi mwaka huu.


Masenza alisema wakati mwaka 2016, washiriki katika maonesho hayo walikuwa 127 ambayo ni sawa na asilimia 42 ya washiriki 300 waliotarajiwa, mwaka huu washiriki wameongezeka hadi 435 sawa na asilimia 87 ya washiriki 500 waliotarajiwa.


Alisema kati ya washiriki hao, washiriki wanne ambao ni wajasiriamali wa viwanda vidogo walitoka nchini Kenya.


Alisema maonesho hayo yalijumuisha maeneo sita ambayo ni pamoja na maonesho ya bidhaa za wajasiriamali na watoa huduma za utalii, kongamano la utalii endelevu, usiku wa Utalii kusini, maonesho ya tamaduni na ngoma asilia, maonesho ya wanyama hai na ziara za kutembelea vivutio mbalimbali.


Katika risala yao iliyosomwa na Daimon Mwenda, wajasiriamali wenye viwanda vidogo walitaja changamoto wanazokumbuna nazo katika kuboresha shughuli zao za uzalishaji.


Changamoto hizo ni pamoja ukosefu wa baadhi ya malighafi ambazo hazizalishwi nchini, mlolongo wa kupata vibali na leseni za uanzishwaji viwanda, mitaji, ushindani na bidhaa toka nje na gharama za ununuzi wa mashine za kodi (EFDs).

=30=

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.