• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

HOFU YASABABISHA WENGI KUTOSAJILI VIFO- RC MASENZA

Posted on: June 11th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Hofu ya matukio ya vifo imesababisha watu wengi kutosajili matukio hayo yanapotokea na kupekelea asilimia 17.5 ya usajili nchini.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua kikao cha hamasa kwa viongozi wa Mkoa wa Iringa kuhusu majaribio ya mpango wa usajili wa vifo, kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.

Masenza alisema kuwa wananchi wamekuwa wakiogopa matukio yanayoambatana na kifo. Woga uliopo ndio unasababisha wananchi wengi kutosajili matukio ya vifo yanapotokea. Woga huyo umesababisha nchi kuwa na wastani wa asilimia 17.5 ya vifo vilivyotokea na kusajiliwa. “Ni imani yangu kwamba tunaenda kubadili hali hii na kama ilivyokuwa kwa usajili wa watoto wadogo ambapo tulikuwa asilimia 11.7 na ndani ya miezi mitatu tukaweza kufika asilimia 100, hivyo naamini tutafanikisha zoezi hili kwa kasi hiyohiyo” alisema Masenza.

Jamii inatakiwa kuhamasishwa kubadili tabia na kuona umuhimu wa kusajili kila tukio la kifo linapotokea. “Wananchi wengi ambao hawana matumizi ya moja kwa moja na cheti cha kifo cha ndugu zao wamekuwa hawafiki RITA kusajili na changamoto kubwa hapa naiona ni kukosa uelewa wa umuhimu wake hivyo kushindwa kubadili tabia” alisema. Ni vigumu kwa mwananchi kuona uhusiano kati ya yeye kusajili kifo cha ndugu yake na maendeleo ya nchi alisema. “Nafahamu zipo nchi ambazo walishaacha kufanya sensa kama tunayofanya kila baada ya miaka kumi na kutumia fedha nyingi kwani nchi hizo wameweka utaratibu ambapo kila mtoto anayezaliwa anasajiliwa na kila mtu anayefariki anasajiliwa hivyo wanakuwa na takwimu za wananchi wake kila siku” alisema Masenza.

Katika kufanikisha zoezi hili, uhamasishaji wa hali ya juu unahitajika alisema mkuu wa Mkoa. Aidha, aliwataka wajumbe wote kuhakikisha ujumbe sahihi unawafikia wananchi ambao wanahitajika kubadili fikra na kuanza kuwa na mtazamo chanya katika usajili wa matukio ya vifo, alisema.

Majaribio ya maboresho ya mfumo wa usajili wa vifo yanafanyika kwa mara ya kwanza katika Mkoa wa Iringa kutokana na mkoa huo kufanya vizuri katika zoezi la usajili watoto wenye umri chini ya miaka mitano na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa.

=30=


Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.