• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

IRINGA DC KUAJIRI WALIMU WA MUDA WA SAYANSI

Posted on: May 24th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Walmashauri ya Wilaya ya Iringa inaajiri walimu wa muda mfupi katika mkakati wa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa walimu wa sayansi.

Kauli hiyo ilitolewa na Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Iringa, Mariam Mlilapi alipokuwa akisoma risala ya utii ya wananchi wa halmashauri ya Wilaya ya Iringa kwa Rais Dkt John Magufuli wakati Mwenge wa uhuru ulipokuwa Tarafa ya Isimani wilayani Iringa.

Mlilapi alisema kuwa halmashauri ya Wilaya ya Iringa ina upungufu wa walimu 145 wa masomo ya sayansi. “Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ina mahitaji ya walimu 381 wa sayansi, waliopo mpaka sasa ni walimu 236 hivyo kuwa na upungufu wa walimu hao 145” alisema Mlilapi. Jitihada zinazofanyika kupunguza changamoto ya walimu wa masomo ya sayansi ni kuajiri walimu wa muda mfupi wa masomo hayo kupitia fedha za fidia ya ada kipengele cha taaluma, aliongeza Mlilapi.

Akiongelea ufuatiliaji na usimamizi wa mifumo ya ithibati na ubora wa elimu, kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Iringa alisema kuwa halmashauri hiyo imekuwa ikifanya ziara katika shule ili kukagua mambo mbalimbali yanayolenga utekelezaji wa sera ya elimu ya taifa. “Ofisi ya mthibiti ubora wa elimu kwa kushirikiana na halmashauri imekuwa ikifuatilia, kusimamia na kuhakikisha ubora wa elimu unaotolewa shuleni unakidhi vigezo vilivyowekwa na serikali, ambapo jumla ya shule za sekondari 15 kati ya 36, shule za msingi 85, kati ya 149 na chuo kimoja cha ualimu zimekaguliwa katika kipindi cha Januari-Mei, 2018” alisema Mlilapi.

Mwenge wa uhuru ukiwa katika halmashauri ya Wilaya ya Iringa umekimbizwa umbali wa Km 218 katika Vijiji saba, Kata saba na Tarafa nne.

Ikumbukwe kuwa halmashauri ya Wilaya ya Iringa ina wakazi 254,032 kwa mujibu wa sense ya mwaka 2012, wanaume wakiwa 123,243 na wanawake 130,789. Tarafa sita, Kata 28, Vijiji 133, Vitongoji 747 na Kaya 60,160.

=30=


Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.