• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

IRINGA IMEANDAA MPANGO WA KUBORESHA UTALII

Posted on: January 18th, 2018


Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

Mkoa wa Iringa umeandaa mpango wa kuboresha maonesho ya utalii karibu kusini ili kuweza kuwavutia watalii wengi kutembelea vivutio vya utalii na kufurahia mandhari iliyopo katika vivutio hivyo.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akiwasilisha taarifa fupi ya Mkoa wa Iringa kwa wajumbe kutoka chuo cha Taifa cha ulinzi waliotembelea Mkoa wa Iringa kwa ziara ya mafunzo.

Masenza alisema kuwa Mkoa wa Iringa ni kitovu cha utalii kwa mikoa ya nyanda za juu kusini. Maonesho ya utalii karibu kusini yanatumika kukuza sekta ya utalii kwa mikoa ya nyanda za juu kusini. “Maonesho ya utalii karibu Kusini yanatumika kama mkakati maalum wa kufungua sekta ya utalii kwa ukanda wa Kusini ambao umejaa fursa na vivutio vya kipee katika utalii. Alitolea mfano maporomoko ya maji ya Kihansi ambapo wanapatikana vyura wa kipekee wanaozaa tofauti na vyura wengine wanaotaga mayai.

Mkoa wa Iringa ukiwa mratibu umeandaa mipango ya kuboresha maonesho haya kwa kutenga eneo la Kihesa Kilolo kama eneo maalum kwa ajili ya maonesho ya utalii karibu kusini. Eneo hili litatumiwa na wadau wa utalii na wadau wa maendeleo kujenga miundombinu kwa ajili ya kuonesha huduma na bidhaa za sekta ya utalii” alisema Masenza.

Mkoa wa Iringa ulifanya maonesho ya kuendeleza utalii ya karibu Kusini kwa miaka miwili mfululizo (mwaka 2016 na 2017) kwa kushirikisha mikoa ya nyanda za juu kusini ya Iringa, Njombe, Mbeya, Ruvuma, Songwe, Rukwa na Katavi.

Akitoa neno la shukrani, kiongozi wa wajumbe kutoka chuo cha Taifa cha ulinzi Capt. Msafiri Hamisi alipongeza kwa mapokezi ya Mkoa na kazi zinazofanywa na Mkoa za kuwahudumia wananchi na kuwaletea maendeleo. Aidha, aliahidi wanafunzi wa chuo cha Taifa cha ulinzi kuwa balozi wazuri kwa mkoa wa Iringa.

=30=



Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.