• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

IRINGA KINARA TUZO YA RAIS UTUNZAJI MAZINGIRA

Posted on: February 9th, 2018

Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Mkoa wa Iringa unatekeleza vizuri mwongozo wa tuzo ya Rais ya utunzaji wa mazingira na uhifadhi ya vyanzo vya maji na Manispaa ya Iringa kushika nafasi ya kwanza kwa Manispaa zote nchini.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akisoma taarifa ya maendeleo ya Mkoa wa Iringa kwa makamu wa Rais mama Samia Suluhu Hassan aliye katika ziara ya siku tano mkoani Iringa jana.

Masenza alisema kuwa Mkoa wa Iringa ulipokea na kutekeleza mwongozo wa tuzo ya Rais ya utunzaji wa mazingira na uhifadhi wa vyanzo vya maji. “Katika mwaka 2015 Manispaa ya Iringa ilishika nafasi ya pili, mwaka 2016 ilishika nafasi ya kwanza kwa Manispaa zote Tanzania na mwaka 2017 ilishika nafasi ya tatu kwa Manispaa zote Tanzania” alisema Masenza.

Akiongelea zoezi la upandaji miti na uhifadhi wa mazingira, mkuu huyo wa Mkoa alisema kuwa Mkoa kwa kushirikiana na wadau wa maliasili umeweza kushiriki kikamilifu katika zoezi la upandaji miti na uhifadhi wa mazingira. Aliyataja mafanikio yaliyopatikana kuwa ni

Kuvuka lengo la upandaji miti 55,000,000 kwa msimu 2016/2017 na kupanda miti 56,108,532. Katika zoezi hilo miti 47,766,366 sawa na asilimia 86.84 ilipona. Juhudi nyingine alizitaja kuwa ni kufanya oparesheni maalum ya kubaini na kuondoa wavamizi na mifugo katika hifadhi ya jamii ya Mbomipa wilayani Iringa. Alisema kuwa oparesheni ilifanyika chini ya kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa ilikamata watuhumiwa 38 wakiwa na mifugo 2,067 na kesi 6 zilifunguliwa mahakamani.

“Halmashauri zote Mkoani Iringa zimetakiwa kuendelea kudhibiti maeneo yote ya hifadhi yasiingizwe mifugo na pia kuendelea kutambua na kupiga chapa mifugo katika maeneo ya Halmashauri ili kuweza kudhibiti mifugo inayoingia bila kufuata taratibu” alisema Masenza.

Kuhusu shindano la usafi wa mazingira lililohusisha halmashauri za majiji, miji na wilaya kwa mwaka 2014, katika ngazi ya Manispaa zote Tanzania, Manispaa ya Iringa ilishika nafasi ya kwanza kitaifa na wilaya ya Mufindi ilishika nafasi ya pili kitaifa wakati kijiji cha Ifunda kikishika nafasi ya kwanza kitaifa.

=30=

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.