• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

IRINGA KUZINDUA KAMPENI YA FURAHA YANGU

Posted on: July 20th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Mkoa wa Iringa umejipanga vizuri kuwahudumia wananchi wote watakaojitokeza katika uzinduzi wa kampeni ya furaha yangu itakayozinduliwa tarehe 24 mjini Iringa.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa mkoa wa iringa, amina masenza alipokuwa akiongea na waandishi wa habari wa mkoa wa iringa kuhusu maandalizi ya uzinduzi wa kampeni ya furaha yangu ofisini kwake leo.

Masenza alisema kampeni hiyo inatarajia kuvuta watu wengi kujitokeza kupima. “Kwa kuwa kampeni hii, itavuta Watu wengi, Mkoa umejipanga tayari kuhakikisha vitendanishi na dawa za ARV zipo za kutosha katika kila kituo kinachotoa huduma hiyo, ili kuweza kuwahudumia vizuri na kuwaanzishia dawa watakaogundulika kuwa na maambukizi ya VVU na UKIMWI”. Watoa huduma watakuwepo wa kutosha kuwahudumia wananchi watakaojitokeza katika uzinduzi wa kampeni hiyo, aliongeza.

Ili tuweze kufanikisha suala hili na ukizingatia ukweli kwamba tuna asilimia kubwa za maambukizi ya VVU.

Mkuu wa mkoa alisema kuwa takwimu zinaonesha kuwa Mkoa wa Iringa una asilimia 11.3 ya maambukizi ya virus vya UKIMWI. “Hivyo, ninatoa wito kwenu waandishi wa habari, kuibeba kampeni hii ya Furaha Yangu, ili iweze kufanikiwa kama ilivyokusudiwa. Ni imani yangu kuwa vyombo vya habari vikibeba kampeni hii kama Agenda muhimu itasaidia katika uhamasishaji wanaume, makundi mengine na jamii kwa ujumla kuweza kujitokeza kupima VVU na watakaogundulika kuanza kutumia dawa za kufubaza VVU mapema” alisema masenza. Wataalam wa Ofisi yangu na wadau mbalimbali wa mapambano ya VVU na UKIMWI wapo tayari kuwapa ushirikiano mtakaouhitaji katika kuandaa na kutengeneza vipindi mbalimbali vitakavyohusiana na Kampeni hii, aliongeza.

Alisema kuwa katika uwanja wa uzinduzi Mwembetogwa, kutakuwa na huduma za ushauri nasaha na upimaji, uchangiaji wa Damu, huduma mkoba za tiba na matunzo, elimu ya tohara kinga kwa wanaume, uzazi wa mpango, kifua kikuu, elimu ya lishe, huduma za bima ya Afya.

Ikumbukwe kuwa uzinduzi wa kampeni ya Furaha yangu kitaifa ya kupima na kuanza kutumia dawa za kufubaza makali ya VVU mapema ulifanywa na waziri mkuu, Kassim Majaliwa tarehe 19, Juni, 2018 mkoani Dodoma. Ikiongozwa na kaulimbiu “Furaha Yangu” – Pima, Jitambue, Ishi.

=30=



Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.