• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

IRINGA NAFASI YA NNE MTIHANI WA DARASA LA SABA KITAIFA

Posted on: July 4th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Mkoa wa Iringa umeshika nafasi ya nne kati ya mikoa 26 katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba kwa mtihani uliofanyika mwaka 2017.

Kauli hiyo ilitolewa na afisa elimu taaluma Mkoa wa Iringa, Mwalimu Farida Mwasumilwe alipokuwa akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya sekta ya elimu Mkoa wa Iringa katika kikao cha wadau wa elimu Wilaya ya Kilolo, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya Wilaya ya Kilolo.

Mwalimu Mwasumilwe alisema kuwa Mkoa wa Iringa umekuwa ukifanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa kumaliza darasa la saba kwa miaka kadhaa. “Kwa mtihani uliofanyika mwezi Septemba, 2017 Mkoa umeshika nafasi ya nne kati ya mikoa 26 ya Tanzania bara ukiwa na ufaulu wa asilimia 83.14 ambapo jumla ya wanafunzi 20,606 wamechaguliwa na kujiunga na kidato cha kwanza 2018, ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2015 ambapo mkoa ulikuwa nafasi ya 10 ukiwa na ufaulu wa asilimia 73.25” alisema Mwalimu Mwasumilwe. Ufaulu umekuwa ukiongezeka kwa halmashauri ya Manispaa ya Iringa na halmashauri ya Wilaya ya Kilolo, aliongeza.

Akiongelea, hali ya miundombinu na samani katika shule za msingi, afisa elimu taaluma mkoa alisema kuwa mkoa una vyumba vya madarasa 4,153, nyumba za walimu 2,203 matundu ya vyoo 7,283 na madawati 99,386. Mkoa umeendelea kuhakikisha miundombinu muhimu na samani vinapatikana katika shule ili kuboresha mazingira ya utoaji elimu, aliongeza.

Akiongelea mikakati ya kukabiliana na upungufu wa miundombinu, afisa elimu taaluma huyo alisema kuwa mkoa umeendelea kutenga fedha kupitia halmashauri zake kutoka katika mapato ya ndani, ruzuku ya serikali na kuwashirikisha wadau wa maendeleo kuchangia ujenzi wa miundombinu ya elimu katika shule za msingi.

Mkoa wa Iringa una jumla ya shule za msingi 499, zikiwa ni ongezeko la asilimia 3.1 mwaka 2018 ikilinganishwa na idadi ya shule 484 mwaka 2015.

=30=



Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.