• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

JAMII KUJENGA UTAMADUNI WA UADILIFU IRINGA

Posted on: July 19th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, IRINGA

Jamii imetakiwa kujenga utamaduni wa uadilifu katika kuitikia sheria ya maadili ya viongozi wa umma na kanuni za serikali za mitaa nchini.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua semina kwa waheshimiwa madiwani na wakuu wa idara na vitengo wanawake katika Mkoa wa Iringa kuhusu maadili ya viongozi wa umma katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.

Masenza alisema kuwa uadilifu sharti ujengwe ndani ya jamii ili kuwa utamaduni wa nchi. “Sheria ya maadili ya viongozi wa umma, kanuni za serikali za mitaa  pamoja na vyombo vya kusimamia utawala bora pekee haviwezi kufanikisha suala la kukuza na kusimamia maadili. Jukumu la kukuza na kusimamia maadili ya viongozi wa umma linahitaji ushirikiano wa pamoja kati ya viongozi, wananchi na wadau mbalimbali” alisema Masenza.

Viongozi wanawake wana dhamana na ushawishi mkubwa katika jamii, hivyo wanapashwa kuongoza katika juhudi za kukuza maadili kwa vitendo. “Hatuna budi kuwahamasisha wananchi kuchukia vitendo vya ukiukwaji maadili na kuwakataa viongozi wasio waadilifu.  Ni matumaini yangu kuwa elimu mtakayoipata katika semina hii mtaitoa pia kwa wanawake wengine katika Halmashauri zenu,  wananchi katika Kata zenu na, Mitaa ambako mnatekeleza majukumu yenu ya kila siku” alisema Masenza.

Moja ya misingi ya demokrasia ni kuwa na Serikali inayowajibika kwa wananchi na yenye viongozi wanaowatumikia wananchi kwa uadilifu, alisema. Wananchi wanategemea viongozi watatumia nafasi zao za uongozi kuwaletea maendeleo na sio vinginevyo, aliongeza. “Sote tunafahamu kwamba uongozi ni dhamana. Kiongozi yeyote, awe ni wa kuchaguliwa ama wa kuteuliwa, amekabidhiwa madaraka na wananchi” alisema. Viongozi wa kisiasa na watumishi wa umma wanatakiwa kutumia nyadhifa zao kwa manufaa ya wananchi.

=30=


Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.