• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

KILIMO KINACHANGIA ASILIMIA 85 YA PATO LA MKOA IRINGA.

Posted on: January 2nd, 2018


Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

Sekta ya kilimo inachangia katika usalama wa chakula na utoaji ajira na uchumi wa Mkoa wa Iringa.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akiwasilisha taarifa fupi ya Mkoa wa Iringa kwa wajumbe kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa waliofanya ziara ya mafunzo ya siku tano mkoani Iringa katika ukumbi wa ofisi ya mkuu wa Mkoa jana.

Masenza alisema “sekta ya kilimo katika Mkoa ni muhimili mkuu wa uchumi na inachangia katika usalama wa chakula na utoaji wa ajira. Sekta hii inachangia takribani asilimia 85 ya pato la Mkoa kwa mujibu wa wasifu wa kiuchumi na Kijamii, mwaka 2013”. Alisema kuwa lengo la Mkoa ni kuhakikisha wananchi wake wanakuwa na chakula cha kutosha, wanaongeza kipato na uhakika wa upatikanaji wa malighafi kwa ajili ya viwanda.

Akiongelea sekta ya mifugo na uvuvi, mkuu wa Mkoa wa Iringa alisema kuwa Mkoa wa Iringa una mashamba makubwa ya mifugo 20 yanayomilikiwa na serikali na watu binafsi. Alisema kuwa mashamba hayo huzalisha maziwa, mitamba na madume bora.

”Mkoa wa Iringa hadi kufikia Juni, 2017 ulikuwa na jumla ya ng’ombe 330,372, mbuzi 160,227, kondoo 62,475, nguruwe 109,131 na kuku wapatao 1,341,718 na eneo linalotumika kwa malisho ni jumla ya hekta 209,003” alisema mkuu wa Mkoa.

Kwa upande wa uvuvi, alisema kuwa Mkoa una mabwawa madogo 1,893 yaliyochimbwa yanayotumiwa kwa shughuli za uvuvi. Alisema kuwa Mkoa una wavuvi 5,807 ambao hufanya shughuli za uvuvi kama mtu mmoja mmoja na katika vikundi. Mavuno ya samaki yamekuwa yakiongezeka kutoka Tani 913.50 mwaka 2011/2012 hadi kufikia Tani 1,186.99 mwaka 2014/15.

Kwa matokeo ya Sensa ya mwaka 2012 Mkoa wa Iringa ulikuwa na watu 941,238 kati ya hao wanaume walikuwa 452,052 na wanawake 489,186 na wastani wa ongezeko la idadi ya watu kwa mwaka ni asilimia 1.1. Makadirio ya idadi ya watu kwa mwaka 2017 ni watu 1,000,040; wanaume wakiwa 480,293 na wanawake 519,747.

=30=



Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.