• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

MAANDAMANO YA AMANI

Posted on: June 24th, 2017

MKOA WA IRINGA WAFANYA MAANDAMANO YA KUMPONGEZA JPM

 Na. Mwandishi Maalum, Iringa

Wananchi wa mkoa wa Iringa wamefanya maandamano makubwa ya amani ya kumpongeza Rais Dk John Magufuli kwa kuimarisha uchumi na kulinda rasilimali za Taifa.

Katika maelezo ya maandamano ya amani ya wananchi wa mkoa wa Iringa yaliyotolewa na mratibu wa maandamano hayo, Paschal Mhongole katika uwanja wa Mwembetogwa  leo asubuhi alisema kuwa wananchi wameamua kuandamana ili kumuonesha Rais Dk Magufuli kuwa wanamuunga mkono katika kuimarisha uchumi na kulinda rasilimali za Tanzania.

Mhongole alisema kuwa baada ya Rais Dk Magufuli kupokea taarifa mbili za kamati za kuchunguza makinikia, yalianza kutolewa maombi kutoka kwa wananchi na makundi mbalimbali juu ya umuhimu wa kufanya maandamano ya amani ya kumuunga mkono Rais Dk Magufuli. “Hivyo wazee waliamua kwenda kumuona mkuu wa mkoa ili kumuomba wananchi kufanya maandamano hayo” alisema Mhongole.

Katika salamu za mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema “katika Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020, inasema kuwa CCM itazielekeza serikali zake kuondoa umasikini, kupunguza tatizo la ajira kwa vijana, kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa na kusimamia amani, ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao”. Alitoa wito kwa wananchi wote kuungana pamoja kumuunga mkono Rais Dk Magufuli ili Mungu aendelee kumlinda na kumpa nguvu na ujasili katika mapambano yake ya kuwakomboa wanyonge wa Tanzania.

Aidha, aliwataka wananchi kufanya kazi kwa bidii. “Kwa wale walio katika ofisi timizeni wajibu wenu. Kwa wale mlio katika sekta binafsi timizeni wajibu wenu ili wote kwa pamoja tukuze uchumi na kuzalisha malighafi zitakazotumika katika viwanda” alisisitiza Masenza.

Katika maoni ya Maria Sangana, mkazi wa Manispaa ya Iringa kuhusiana na utendaji kazi wa Rais Dk Magufuli, alisema kuwa Rais Dk Magufuli ni mchapa kazi hodari na ni chachu kwa watumishi wengine na wananchi kwa ujumla kuinga utendaji wake ili kukuza uchumi wa Tanzania. “Hata ukiangalia tu muitikio wa wananchi katika maandamano haya ni mzuri. Hii inaashiria kuwa wananchi wengi wanamuunga mkono Rais wetu. Hata ukiangalia ujumbe ulioandikwa katika mabango unasadifu imani waadamanaji waliyonayo kwa Rais” alisisitiza Sangana.

=30=



Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.