• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

MASENZA AWATAKA WAFANYA BIASHARA KULIPA KODI

Posted on: February 21st, 2018

Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Serikali mkoani Iringa imewataka wafanyabiashara wote kulipa kodi kwa mujibu wa sheria ili serikali iweze kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akisalimia wachimbaji wadogo wa mgodi wa nyakavangala katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Nyakavangala kilichopo wilayani Iringa alipokuwa akiongea na wachimbaji wadogo wakati wa ziara ya naibu waziri wa Madini, Dotto Biteko mkoani Iringa jana.

Masenza alisema “katika Mkoa wangu, siruhusu mtu yeyote kufanya biashara bila kulipa kodi. Lazima kulipa kodi. Kodi ndiyo inajenga zahanati, kodi ndiyo inajenga shule na miundombinu yote na kodi ndiyo inalipa mishahara”. Alisema kuwa utamaduni wa kulipa kodi ndiyo utawezesha ujenzi wa barabara ya kuelekea katika machimbo ya Nyakavangala kwa kiwango kinachoridhisha.

Aidha, pamoja na kuwapa pole wachimbaji wa dhahabu wa Nyakavangala kufuatia vifo vilivyotokana na ajali zilizotokea siku za nyuma katika mgodi huo, aliwataka kuzingatia kanuni za usalama. “Sitaki vifo katika Mkoa wangu. Lazima kanuni za usalama zizingatiwe wakati wa uchimbaji wa dhahabu”. Alisema kuwa ushauri wa wakaguzi wa madini uzingatiwe ili machimbo ya Nyakavangala yawe eneo salama kwa wachimbaji wadogo mkoani Iringa.

Wakati huohuo, mkuu wa Mkoa wa Iringa alimuagiza mkuu wa Wilaya hiyo kwenda kuwasikiliza wananchi waliojaribu kubeba mabango katika ziara ya naibu waziri wa Madini ili kufahamu hoja zao na kuzitafutia ufumbuzi.

Akiongea katika majumuisho ya ziara yake yaliyofanyika katika ofisi ya mkuu wa Mkoa, naibu waziri wa Madini, Dotto Biteko alisema kuwa nchi imempata kiongozi anayethubutu kuhakikisha madini yanawanufaisha watanzania. “Rais, Dr John Magufuli ana dhamira ya dhati kuyafanya madini yawanufaishe wananchi wa Tanzania na kuchangia katika pato la taifa. Dhamira yake ni kuona madini yanawanufaisha wachimbaji wadogo na hatimae kufikia hatua ya uchimbaji mkubwa” alisema Biteko.

=30=



Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.