• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

Mkuu wa Mkoa Iringa atoa maagizo mazito kwa Jamii Kupambana na Ukatili kwa Wanawake na Watoto

Posted on: January 16th, 2020

Mkuu wa Mkoa Iringa atoa maagizo mazito kwa Jamii Kupambana na Ukatili kwa Wanawake na Watoto, Atoa Maelekezo kwa Wakuu wa Wilaya na Wadau Mbalimbali

Akitoa maelekezo hayo katika kikao kilichoandaliwa na Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa kushirikiana na Wizara ya Afya Jinsia na Wanawake na Watoto, Mheshimiwa Ally Hapi amesema, kuna umuhimu wa kupitia upya waganga wote wa jadi waliopo Mkoani humo, kuacha mila na desturi zilizopitwa na wakati, kuacha mambo ya kishirikina na ulevi wa kupindukia.

Mheshimiwa Hapi amesema mambo haya huchangia sana kufanya ukatili kwa wanawake na watoto. Akitoa mfano akasema mwanaume akishalewa anaweza kumpiga mke wake bila sababu. Utamaduni wa kupiga mwanamke umepitwa na wakati, mwanamke anatakiwa kupewa mapenzi, kubembelezwa na kupewa mahaba. Pia mtu akishaenda kwa mganga wa jadi kutafuta utajiri, ataambiwa akabake mtoto.

Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Watoto wameandaa mpango unaoitwa MTAKUWWA, ambao unafadhiliwa na UNICEF, mpango huu wa mawasiliano utasaidia kupunguza ukatili kwa wanawake na watoto. Pamoja na jitihada za UNICEF lazima jamii ipewe elimu juu ya mambo haya ya ukatili wa wanawake na watoto.

Ameongeza kuwa, hata wanaume huwa wanafanyiwa ukatili japo huwa hawasemi. Pia wazazi hatuna desturi za kuangalia watoto wetu pindi wanapotoka shule au kucheza sehemu mbalimbali. Kwani imebainika kuwa asilimia kubwa watoto hubakwa, kulawitiwa wakiwa wanatoka kwenye masomo ya ziada (Tuition), vibanda wanavyoonesha sinema na hata kumtuma mtoto nyakati za usiku kwenda dukani au sehemu mbalimbali.

Amesisitza tena, kila shule kuwe na mwalimu wa malezi ambaye atakuwa akiwaangalia na kuwasikiliza watoto pindi wanapokuwa wamepatwa na jambo kama hili. Hii itasaidia watoto kueleza matatizo yao bila uoga.

Ameongeza kwa kusema kuwa, nilipoenda kutembelea gerezani, wafungwa 30 waliofungwa maisha kwa kesi za kufanya ukatili. Pia takwimu za ubakaji, ulawiti na ukatilili wa kingono kuanzia Januari hadi Novemba, 2019 kesi zilizojulikana ni watoto 404 na wanawake 37 ambao wamefanyiwa ukatili. Jambo hii la ukatili linasababisha ongezeko la maambukizi ya UKIMWI, kwani Mkoa upo katika nafasi ya 11.3% na 43% ya udumavu hivyo bado tuna kazi kubwa ya kupambana vita hivi. Tatizo hili linachangiwa na mambo ya mila na desturi, Ushirikina, ulevi wa kupindukia.

Mwisho Mheshimiwa Hapi amesisitiza kuwa, jamii na wadau itoe macho katika maeneo ya kuonesha sinema, kwenye masomo ya ziada (tuition), waganga wa jadi ili ijulikane nini kinaendelea katika maeneo hayo.


Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.