• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Ally Hapi awataka Waajiri kupeleka michango ya wanachama katika Mifuko ya Jamii na kuhimiza Sekata Isiyo Rasmi kujiunga na Mfuko huo.

Posted on: February 11th, 2020

Mheshimiwa Hapi ameyasema hayo katika semina iliyoandaliwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) iliyofanyika Mjini Mafinga Februari 10, 2020.

Akifungua semina hiyo Mheshimiwa Hapi amesema, ‘mtakumbuka tulikuwa na mashirika mengi sana ya Hifadhi ya Jamii ikiwemo LAPF, NPF, EGPF nk, lakini SErikali imeamua kuunganisha mashirika hayo na kuwa mfuko mmoja ambao utahudumia wafanyakazi wa Serikali ambao kwa sasa baada ya kuunganishwa unaitwa PSSSF, na NSSF imebaki kuhudumia wafanyakazi wa Sekta Binafsi. Sheria hii inamtaka Mwajiri kupeleka michango ya mwanachama kila mwisho wa mwezi bila kukosa na bila kuchelewesha. Kwani baadhi ya Waajiri wamekuwa wakichelewesha michango ya wanachama, lakini sasa Serikali imeweka sheria kali kuwa, Mwajiri akichelewesha michango atapata faini, na asipopeleka kabisa basi atapata penati.

Ameongeza kuwa, Sekta zisizo rasmi kama bodaboda, Mama Nitilie, na wajasiriamali wengine wadogo wadogo wanatakiwa kuwa wanachama wa mfuko ili kujiwekea akiba. Hii itasaidia kuwainua wafabiashara/wajasiriamali katika kukuza uchumi, kwani sekta hii isiyo rasmi ina mchango mkubwa sana katika Taifa.

Tanzania imeingia katika ubora wa mazingira mazuri ya uwekezaji kwa wajariamali wadogo, tumekuwa nchi ya 21 duniani katika ubora huo ikiongozwa na India ikifuatiwa na China. Hivyo tuna nafasi kubwa sana ya kuwaendeleza wajasiriamali hawa ili kukuza uchumi wa Taifa. Katika Mkoa huu tumetoa vitambulisho 60,000 kwa wajasiriamali na tumepata zaidi ya bilioni 1, itakuwaje kwa Tanzania nzima?

Wito kwa NSSF, ni muhimu kuwafikia wajasiriamali wote  60,000 wa mkoa huu, pia mnawaelekeza faida za mfuko kama matibabu, mikoo baada ya kustaafu, mafao ya uzazi nk.

Pia ameongeza kwa Waajiri kuwa, hakikisheni michango inaenda kwenye mifuko kwa wakati, watu wanaostaafu wapate mafao yao kwa wakati, tena mjivunie wastaafu, kwani mkiwalipa kwa wakati wataipatia sifa njema mfuko. Hii itasaidia kuokoa wastaafu kukopa fedha katika mashirika yenye riba kubwa (fedha za moto). Waajiri wahakikishe watumishi wote wamejiandikisha kwenye mfuko.

Pamoja na semina ya NSSF, Mheshimiwa Hapi amepata nafasi ya kukabidhi majengo yaliyokuwa yanatumika na Kampuni ya Wachina ya kutengeneza barabara, na kuwa Kituo cha Afya cha Changarawe Mjini Mafinga. Majengo hayo yenye ofisi na nyumba 8 za watumishi yatasaidia kuondoa msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Mji Mafinga.

Pia ametembelea mradi wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Mufindi na kujionea ujenzi unaondelea. Japo kuna mapungufu katika umaliziaji ambao unatokana na ucheleweshwaji wa vifaa Mheshimiwa Hapi ametoa siku kumi na nne kukamilisha ujenzi huo.

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.