• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

MUITIKIO WANAUME KUPIMA VVU SI WA KURIDHISHA

Posted on: July 9th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Watanzania zaidi ya asilimia 50 ya watu wanaoishi na VVU hawajui kuwa wanaishi na VVU mchango mkubwa ukitokana na kiwango cha wanaume kutojitokeza kupima VVU.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua kikao cha maandalizi ya kampeni ya Furaha Yangu, ya kupima VVU na kuanza dawa mapema, kilichofanyika katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa.

Masenza alisema “kitaifa inakadiriwa kuwa asilimia 52.2 ya watu wanaoishi na VVU hawajui kuwa wanaishi na VVU. Kwa kiasi kikubwa hali hii inachangiwa na wanaume ambao kiwango chao cha upimaji kiko chini sana, ambacho ni asilimia 45.3 ukilinganisha na kinamama ambao kiwango chao ni asilimia 55.9 kulingana na matokeo ya utafiti wa viashiria vya VVU/UKIMWI (Tanzania HIV Impact Survey 2016/17)”. Umefika wakati kampeni za mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU zielekezwe katika kuwahamasisha wanaume/vijana wa kiume kupima VVU na magonjwa mengine, aliongeza. “Najua jambo hili si jepesi kutokana na hulka za akina baba na mazoea ambayo tayari yameshajengeka katika familia nyingi za kiafrika Tanzania ikiwemo” aliongeza Masenza.

Aidha, alitoa wito kwa akina mama walio katika ngazi za uongozi kuhamasika na kuwahamasisha akina mama wanaowaongoza kuwa na agenda moja ya kuwaunga mkono wanaume na vijana wa kiume kuwa tayari kujitokeza kupima afya zao.  

Vilevile, aliwaagiza viongozi ngazi zote mkoani Iringa kutumia kauli mbiu aliyoiongoza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayowalenga wanaume isemayo “Mwanaume Jali Afya Yako, Pima VVU”  ili kuweka msisitizo katika ushiriki wa wanaume katika kampeni hiyo.  

Uzinduzi wa kitaifa wa kampeni ya “Furaha Yangu” umedhihirisha azma ya Serikali yetu ya awamu ya tano ya kuhakikisha kuwa inaimarisha na kuongeza kasi ya mapambano, ili baada ya kuzifikia hizo “tisini tatu” mwelekeo sasa unabaki ni ule wa kufikia zile “sifuri tatu”; kutokuwepo kwa maambukizi mapya ya VVU, kutokuwepo kwa unyanyapaa kwa watu wanaoishi na VVU, na kutokuwepo na vifo vinavyotokana na UKIMWI ifikapo mwaka 2030.

=30=

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.