• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

RC HAPI AANZA ZIARA WILAYA YA KILOLO

Posted on: August 13th, 2018


Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi ameanza ziara ya kutembelea Wilaya za Mkoa wa Iringa, akianza na Wilaya ya Kilolo.

Akiwa Wilayani Kilolo, alifanya kikao na Kamati ya Ulinzi na Usalama na kusisitiza umoja na mshikamano. Vilevile, aliitaka Kamati hiyo kuweka utaratibu wa kubadilishana taarifa kwa wakati ili ziwawezeshe kufanya maamuzi sahihi katika kazi zao.

Mkuu wa Mkoa alitembelea ofisi ya CCM Wilaya ya Kilolo na kufanya kikao na kamati ya siasa ya Wilaya hiyo. Aliomba ushirikiano katika kuijenga Iringa mpya. Aidha, aliomba umoja na ushirikiano kuendelea kudumishwa kwa mkuu we Wilaya, Mkurugenzi na wakuu wa idara katika kutekeleza Ilani ya CCM.

Mkuu wa Mkoa alifanya kikao na watumishi wa Wilaya ya Kilolo na kuwataka kuwa wamoja. "Natamani kujenga Iringa mpya yenye umoja, umoja baina ya viongozi na watumishi. Tunapanga pamoja na tunatekeleza pamoja. Msitangulize ubinafsi wenu bali tangulizeni umoja wenu" alisisitiza mhe Hapi.


Aidha, aliwataka watumishi kutambua kuwa vyeo vyao ni dhamana ambazo wamepewa kwa ajili ya kuwatumikia wananchi. "Kila mmoja lazima awaheshimu wananchi wa Kilolo. Tusiwajibu ovyo, wala kuwa na kiburi. Tuwasikilize na kuwahudumia. Wananchi hawa ndiyo walipa kodi na wanaotulipa mishahara" alisisitiza mhe Hapi.


Mkuu wa Mkoa alisisitiza uadilifu na kufanya kazi kwa haki na kuzingatia sheria. Alikemea vitendo vya rushwa na kusisitiza utunzaji wa siri za ofisi.

Mhe Hapi aliitaka halmashauri ya Wilaya ya Kilolo kujikita katika ukusanyaji mapato na kudhibiti matumizi yasiyo ya lazima ya fedha za serikali.


Katika kikao na wazee wa Wilaya ya Kilolo, Mkuu wa Mkoa aliwataarifu wazee hao kuwa alienda kujitambulisha kwao na kuomba ushirikiano wao katika kufikia malengo ya serikali. Aliwahakikishia wazee hao kuwa watendaji wa serikali wataendelea kutoa huduma nzuri kwa wananchi ili waendelee kuiunga mkono nakuiamini serikali yao. "Nimewaagiza watendaji kuwafuata wananchi huko mlipo na siyo nyie kuja kuwafuata watendaji walipo" alisisitiza mhe Hapi.

Katika mkutano wa hadhara, aliwahakikishia wananchi kuwa watendaji watawahudumia na kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi kwa wakati. Aliwataarifu wananchi kuwa amewaagiza watendaji wa serikali kutoka ofisini na kuwafuata Wananchi katika maeneo yao na kutatua kero zao.

Mkuu wa mkoa yupo katika ziara yake ya wilaya kwa wilaya kwa lengo la kujitambulisha na kuelezea mwelekeo wa ujenzi wa Iringa mpya anayokusudia katika uongozi wake.

=30=

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.