• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

RC HAPI AKATAA KUWEKA JIWE LA MSINGI KLINIKI YA UZAZI NA AFYA YA MTOTO MUFINDI

Posted on: September 9th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi amekataa kuweka jiwe la msingi jengo la kliniki ya uzazi na afya ya mtoto katika kituo cha afya Mgololo, wilayani Mufindi  baada ya kutoridhishwa na gharama kubwa za ujenzi zilizotumika.

Akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya Tarafa kwa Tarafa ya kutembelea Tarafa 15 za Mkoa wa Iringa, iliyoanzia katika Tarafa ya Kasanga Wilaya ya Mufindi, alipangiwa kutembelea na kuweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la kliniki ya uzazi na afya ya mtoto. Mhe Hapi alikataa kuweka jiwe la msingi baada ya kukagua ujenzi wa jengo hilo lililogharimu kiasi cha shilingi milioni 360. “Siwezi kuweka jiwe la msingi katika jengo hili. Nataka kujiridhisha na thamani ya fedha katika mradi huu. Mnapotengeneza makadirio ya gharama za ujenzi wa mradi (BOQ) makubwa mnamkatisha tamaa muwekezaji. Nataka maelezo kutoka Wakala wa ujenzi Tanzania (TBA) nani kaandaa makadirio ya gharama za ujenzi wa mradi huu” alihoji Mhe Hapi. Maeneo mengi tumejenga Zahanati kwa gharama za shilingi milioni 400, iweje jengo hili tu la kliniki ya uzazi na afya ya mtoto ligharimu shilingi milioni 360, aliendelea kuhoji, Mhe Hapi.

Akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa jengo la kliniki ya uzazi na afya ya mtoto, katika kituo cha afya Mgololo kwa Mkuu wa Mkoa, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Dkt Fredrick Mugarula alisema kuwa ili kukamilisha ujenzi wa jengo la kliniki hiyo, imekadiriwa kutumia kiasi cha shilingi milioni 360. “Serikali kupitia ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa na TBA wameweza kutoa marekebisho ya ramani na makisio ya ujenzi” alisema Dkt Mugarula.

Akiongelea matarajio ya mradi huo, alisema kuwa baada ya ujenzi kukamilika, Halmashauri inatarajia kuwa na ongezeko kubwa la wateja katika kliniki hiyo kutokana na mazingira yenye kutoa huduma bora. Aidha, hali hiyo itapunguza vifo vya kina mama na watoto vilivyokuwa na uhusiano wa kutopata huduma bora za afya.

Kituo cha afya Mgololo ni miongoni mwa vituo tisa vya afya vinavyotoa huduma katika Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, kikiwa kilianzishwa mwaka 1985 na Baba wa Taifa Mwl Julius Nyerere kama sehemu ya kiwanda cha karatasi Mgololo.

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • KUELEKEA MBIO ZA THE GREAT RUAHA MARATHON

    July 01, 2025
  • MAAFISA ELIMU WAAGIZWA KUSIMAMIA MAENDELEO YA MICHEZO MASHULENI

    June 29, 2025
  • MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 YACHAGIZA UCHUMI WA IRINGA.

    June 29, 2025
  • KARIBU MKOANI IRINGA

    June 28, 2025
  • View All

Video

MAENDELEO KWA SASA BILA MAWASILIANO HAYAWEZEKANI- RC KHERI
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.