• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

RC HAPI AWATAKA WAFANYAKAZI KUTOA TAARIFA ZA KAZI KILA WIKI

Posted on: August 14th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Wafanyakazi wilayani Mufindi wametakiwa kutoa taarifa ya utekelezaji wa majukumu yao kila wiki yakionesha jinsi walivyotatua kero za wananchi katika maeneo yao.

Agizo hilo lilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe Ally Hapi alipokuwa akiongea na wafanyakazi wa Wilaya ya Mufindi katika ukumbi wa CCM mjini Mafinga leo.

Mhe Hapi alisema kuwa kila wiki mfanyakazi atoe taarifa ya kazi alizofanya na kazi anazotarajia kufanya wiki inayofuata. “Nataka tuwe na mfumo wa utoaji taarifa za utendaji kazi wa serikali kwa wiki, ili tujue nani anafanya kazi na wasiofanya kazi tuwajue. Wakuu wa idara na vitengo mwisho wa siku tutajua matokeo ya utendaji kazi yapoje ili mwisho wa mwezi tupate mishahara kihalali” alisisitiza mhe Hapi. Katika utekelezaji wa agizo hilo, wakurugenzi wa halmashauri ya mji wa Mafinga na Wilaya ya Mufindi waliagizwa kusimamia utekelezaji huo. Aidha, aliwakumbusha wafanyakazi hao kuwa kipimo cha kazi wanazofanya ni utatuzi wa migogoro na kero za wananchi.

Mkuu wa mkoa alisema kuwa anatamani kuona kero za wananchi zinaisha katika mkoa huo. Wafanyakazi wa serikali wanajukumu la kumsaidia mhe Rais kufikia malengo ya nchi. “Kama mhe Rais anafanya ziara mkoani Iringa na anapokelewa na mabango ya malalamiko maana yake wafanyakazi hamumsaidii Mhe Rais. Natamani kuona Mhe Rais anapokelewa kwa mabango yanayopongeza utendaji kazi wake na juhudi zake za kuiletea maendeleo nchi” alisema Mhe Hapi.

Mkuu wa mkoa alisema kuwa anategemea kufanya ziara ya siku 18 ya kutembelea tarafa kwa tarafa. “Nitatembelea miradi ya maendeleo na kufanya mikutano mitatu kwenye kila tarafa. Katika ziara hiyo nitasikiliza kero za wananchi na kila mfanyakazi atajibu kero za wananchi kulingana na eneo lake. Kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe, sitajibu kwa niaba ya mfanyakazi” alisisitiza Mhe Hapi. Aliongeza kuwa kutokana na wafanyakazi kutotimiza majukumu yao, wamekuwa wakizalisha chuki kwa serikali iliyo madarakani kutokana na kushindwa kutatua shida za wananchi. Alisisitiza kuwa hatakuwa tayari kuwavumilia wafanyakazi wanaozalisha chuki na kuifanya serikali ya awamu ya tano ichukiwe na wananchi.

Aliwataka watendaji kuwaheshimu na kuwasikiliza wananchi. “Kumekuwa na tabia ya kuwadharau wananchi na kuwajibu ovyo wanapohitaji huduma katika ofisi zetu. Watendaji ngazi ya vijiji, kata na ngazi zote lazima watenge siku ya kusikiliza kero za wananchi”, alisema.

Mhe Hapi aliwataka wafanyakazi wa serikali kufanya kazi kwa kutenda haki na kutunza siri za serikali. “Wafanyakazi lazima kutenda haki na kuwa waadilifu katika maamuzi yenu. Rushwa na migogoro tujiepushe nayo. Tufanye maamuzi kwa haki kwa maslahi ya wananchi wa Mufindi” alisema mhe Hapi. Aliwakumbusha wafanyakazi hao kuwa kutunza siri za ofisi ni sehemu ya uadilifu.

Mkuu wa mkoa wa Iringa yupo katika siku ya pili ya ziara yake ya kutembelea wilaya za mkoa wa Iringa na kufanya vikao na wafanyakazi na wazee kuelezea dira ya uongozi wake katika falsafa yake ya ujenzi wa Iringa mpya.

=30=


Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.