• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

RC MASENZA ASHAURI MATUMIZI YA TEHAMA MAHAKAMA KUU IRINGA

Posted on: January 30th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza ameishauri Mahakama kuu kanda ya Iringa kuongeza kasi ya matumizi ya Tehama katika utoaji wa haki kwa wananchi.

Kauli hiyo aliitoa katika salamu zake kwenye uzinduzi wa wiki ya sheria nchini uliofanyika katika uwanja wa Mahakama kuu Iringa jana.

Masenza alisema kuwa faida za Tehama katika Mahakama ni kurahisisha utoaji haki kwa wakati kwa wananchi. Aliongeza kuwa Tehama inasaidia kutunza kumbukumbu muhimu za mwenendo wa kesi na hatimae utolewaji wa haki. “Tehama inaimarisha mawasiliano miongoni mwa wadau. Ni rahisi kuwapa taarifa wadau huko waliko wakahudhuria Mahakamani kwa wakati pale wanapohitajika bila taarifa kupotea. Tehama huimarisha maadili ya utoaji wa haki kwa wananchi, vifaa kama CCTV camera na vifaa vingine vya aina hiyo ni muhimu katika kuimarisha maadili ya haki” alisisitiza Masenza.

Katika hotuba ya Jaji mfawidhi wa Mahakama kuu kanda ya Iringa, mheshimiwa Mary Shangali alisema kuwa wiki ya sheria nchini imelenga Mahakama kujipambanua kwa wananchi na kueleza majukumu ya Mahakama na kutoa elimu kwa wananchi kuwa mahkama kuu ya Tanzania ipo kwa ajili ya wananchi na haki zao.

Mheshimiwa Shangali aliongeza kuwa wiki hiyo inalenga kupima utendaji kazi wa Mahakama. Alisema katika maadhimisho hayo, vituo vya kutolea elimu na kupokelea maoni ya wananchi vimeandaliwa katika shule ya sekondari ya wasichana Iringa, shule ya sekondari ya Miyomboni na chuo kikuu cha Iringa.

=30=    

  

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.