• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

Rushwa Iringa kuwa Historia- Prof Kahyarara

Posted on: April 27th, 2018

Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini (TAKUKURU) mkoa wa Iringa imetakiwa kuhakikisha rushwa inakuwa historia mkoani hapa kwa kushughulikia taarifa za malalamiko ya rushwa kutoka kwa wananchi ili waendelee kuwa na Imani na taasisi hiyo.

Rai hiyo imetolewa na mkurugenzi mkuu wa NSSF Prof Godius Kahyarara alipotembelea banda la TAKUKURU katika maonesho ya shughuli na huduma za wafanyakazi yanayoendelea katika uwanja wa Kichangani mjini Iringa jana.

Prof. Kahyarara alisema kuwa TAKUKURU ina wajibu wa kuhakikisha rushwa inakomeshwa mkoani Iringa ili wananchi waweze watekeleza majukumu yao. Alisema kuwa rushwa imekuwa ikikwamisha maendeleo ya wananchi na kuwanyima haki ya kupata huduma. “TAKUKURU mnawajibu wa kuifanya Iringa kuwa eneo huru dhidi ya rushwa. Na huu ndiyo wajibu wenu wa msingi” alisema Prof. Kahyarara.

Awali afisa muelimishaji wa TAKUKURU mkoa wa Iringa, Aneth Mwakatobe alieleza kuwa hali ya rushwa mkoani Iringa imeendelea kushuka katika miaka ya hivi karibuni. Alisema kuwa hali ya rushwa imeendelea kushuka mkoani hapa kutokana na uelewa wa wananchi kuwa mkubwa. “TAKUKURU mkoa wa Iringa imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi kuhusiana na jinsi ya kukabiliana na rushwa. Katika kuonesha uelewa mkubwa kwa wananchi, wananchi wameendelea kutoa taarifa kwetu na kusaidia uchunguzi kufanyika na kutoa matokea chanya” alisema Mwakatobe.

Afisa huyo aliyataja maeneo yanayolalamikiwa kuwa na vitendo vingi vya rushwa ni yale ambayo watoa huduma wake wanakutana na wananchi moja kwa moja. Alitolea mfano wa maeneo hayo kuwa ni halmashauri, polisi, mahakama, ardhi, na afya.

TAKUKURU ni moja ya waoneshaji wa huduma katika mabanda ya maonesho ya Mei Mosi kitaifa yanayofanyika katika viwanja vya kichangani mjini Iringa yakitangulia sherehe ya Mei Mosi kitaifa itakayohudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.

=30=

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.