• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

Serikali kutatua kero za Wafanyakazi- Dkt Magufuli

Posted on: May 1st, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Serikali ya awamu ya tano itaendelea kushughulikia kero za wafanyakazi na kuboresha maslahi ili wafanye kazi kwa kujituma na tija zaidi.

Kauli hiyo ilitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli alipokuwa akihutubia mamia ya wafanyakazi waliofurika katika uwanja wa michezo wa Samora mjini Iringa katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani.

Dkt Magufuli alisema kuwa serikali yake itaendelea kushughulikia kero na kuboresha maslahi ya wafanyakazi nchini. “Leo ni siku ya wafanyakazi, napenda kutumia fursa hii kuwapongeza wafanyakazi kwa mchango wenu mkubwa wa kuiletea nchi maendeleo. Hongereni sana”. Aidha, aliwataka watumishi hao kutanguliza nidhamu na uwajibikaji katika utendaji wao wa kazi. “Mtumishi akiwa mvivu na mzembe anakuwa ni mnyonyaji” alisema Dkt. Magufuli.

Kuhusu wafanyakazi kuhamishwa bila kulipwa stahili zao, Rais Dkt Magufuli alimuagiza waziri mkuu kuwasimamia wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa ambao bado wanahamisha wafanyakazi bila kuwalipa stahili zao. “Waziri mkuu nakuomba ulisimamie hilo. Hatuwezi kuwa tunatoa maagizo halafu mtu mwingine aendelee kufanya hivyo. Tulishatoa maagizo mtu asihamishwe bila kulipwa. Naagiza tena viongozi ndani ya serikali wasihamishe bila kulipa fedha za uhamisho. Ni matumaini yangu sitarudia tena kuzungumzia hili katika maisha yangu”.

Akiongelea malimbikizo ya watumishi, alisema kuwa serikali yake imelipa malimbikizo kwa watu 52,852 yenye thamani ya shilingi bilioni 86,323. Vilevile, aliwahakikishia watumishi kuwa wale wote wenye madai halali watalipwa haki zao. “Kwa hizi nyuso za furaha mnazonionesha leo, ningekuwa na hela kwenye chungu zimebaki pale, leo ningetamka tu. Lakini nikitamka ntazitoa wapi? Nina mpango wa kuajiri wafanyakazi 52,000 ntawalipa nini? Dhamira yangu inanituma kwamba kusubiri ni kitu kizuri. Hebu tujenge miundombinu na kuajiri hawa 52,000. Tutaendelea kulipa viporo vya madeni hadi viishe” alisema Dkt Magufuli.

=30=

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • KUELEKEA MBIO ZA THE GREAT RUAHA MARATHON

    July 01, 2025
  • MAAFISA ELIMU WAAGIZWA KUSIMAMIA MAENDELEO YA MICHEZO MASHULENI

    June 29, 2025
  • MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 YACHAGIZA UCHUMI WA IRINGA.

    June 29, 2025
  • KARIBU MKOANI IRINGA

    June 28, 2025
  • View All

Video

MAENDELEO KWA SASA BILA MAWASILIANO HAYAWEZEKANI- RC KHERI
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.