• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

VIBALI ZIARA ZA KIELIMU KULINDA HAKI ZA WATOTO IRINGA-RC MASENZA

Posted on: June 7th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Serikali mkoani Iringa imetoa maelekezo kuwa vibali vyote vya ziara za elimu ziwe na mkakati wa kulinda haki za watoto dhidi ya ukatili wa aina yoyote.

Maelekezo hayo yalitolewa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Mwl Amina Masenza katika hotuba yake kwenye kilele cha maadhimisho ya wiki ya kusoma ngazi ya mkoa yaliyofanyika katika mji mdogo wa Ilula wilayani Kilolo.

Mwl Masenza aliitaka jamii nzima kuwa na sauti ya watoto kuripoti matukio yanayoashiria unyanyasaji wa watoto wote. “Ninaagiza vibali vyote vya ziara zote za kielimu zinazofanyika katika mkoa wetu ziwe na mkakati maalum wa kulinda haki za watoto na kuhakikisha hakuna ukatili wa aina yoyote unaofanyika kwa watoto wetu, kinyume na hapo kisitolewe kibali cha shughuli hizo” aliagiza Mwl Masenza. Vilevile, alizitaka shule zote zenye vyombo vya usafiri kuhakikisha wanapowarudisha watoto kunakuwa na usimamizi makini ili watoto wakubwa wasipate fursa ya kuwanyanyasa watoto wadogo katika vyombo vya usafiri.

Aidha, mkuu wa Mkoa aliwataka walimu kuzingatia nidhamu, uadilifu na uwajibikaji katika maeneo yao ya kazi. “Walimu mnawajibika kwa wanafunzi, kwa jamii kwenye kazi zenu, kwa mwajiri na taifa kwa ujumla. Wajibu wenu walimu ni kumlea mwanafunzi kiakili, kimwili na kiroho ili awe raia mwema na mzalendo wa nchi yetu” alisisitiza Mwl Masenza. Aliwataka walimu kujiepusha na ulevi, wizi, uasherati, rushwa na ubaguzi katika maeneo ya kazi.

Taarifa ya maadhimisho ya wiki ya kusoma Mkoa wa Iringa iliyowasilishwa na kaimu afisa elimu Mkoa wa Iringa, Mwl Farida Mwasumilwe alisema kuwa mpango wa kukuza stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK) umepata mafanikio makubwa mkoani hapa. Alisema mpango huo umefanikiwa kuwapatia mafunzo ya stadi za KKK walimu 3,796 kati ya walimu 5326 sawa na asilimia 71.3. Mafanikio mengine aliyataja kuwa idadi ya wanafunzi wasiojua KKK imeshuka. Mkoa una wanafunzi 34,282 kati ya 38,562 wa darasa la pili wanajua kusoma sawa na asilimia 88.91, wanafunzi 4,279 hawamudu KKK. Uwepo wa vitabu vya ziada na kiada kwa stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu, aliongeza Mwl Mwasumilwe. Mafanikio hayo yamechangiwa na juhudi za serikali za kukabiliana na changamoto za wanafunzi kutojua kusoma. Pia uwepo wa wa miradi mikubwa miliwi inayoendesha mafunzo ya KKK katika mkoa ambayo ni LANES na TUSOME PAMOJA.

Maadhimisho ya wili ya kusoma Mkoa wa Iringa yalitanguliwa na maadhimisho hayo katika ngazi za halmashauri kuanzia tarehe 31 Mei, 2018 hadi 6 Juni, 2018.

=30=


Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.