• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

WATOTO WANAOISHI MAZINGIRA HATARISHI WATAKIWA KUSOMA KWA BIDII

Posted on: June 12th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Watoto wanaoishi katika mazingira magumu wametakiwa kusoma kwa bidii ili wawe kielelezo kwa watoto wengine nchini.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipoongoza kikundi cha kina mama cha Utulivu kutembelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu wanaolelewa na kituo cha Dar Bilal na kuwapa zawadi za sikukuu ya Idi El Fitri mjini Iringa.

Masenza alisema kuwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu hawajatengwa na jamii. Serikali inawatambua na itaendelea kusimamia ustawi wao ili waweze kukua na kupata elimu kama watoto wengine. Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Magufuli imeanzisha mpango wa elimu msingi bila malipo ili watoto wote wa kitanzania waweze kunufaika na elimu hiyo, alisema. “Elimu dunia ni muhimu sana kwa watoto katika kufanikisha juhudi za serikali za kuhakikisha kila mtoto anapata elimu nchini na kutoa mchango wake katika maendeleo ya taifa” alisema Masenza.

Awali mwenyekiti wa kikundi cha kina mama cha Utulivu, Sada Hassan alisema wakina mama wanawajibu wa kuwa karibu na watoto sababu wao ndiyo wazazi. Kina mama wanawajibu wa kuwalea na kuwalinda watoto pasipo kujali changamoto zinazojitokeza katika maisha yao, aliongeza.

Nae msimamizi wa makao ya watoto ya Dar Bilal, Ally Hassan alisema kuwa makao hayo yanakabiliwa na changamoto ya vifaa vya shule. Alitoa wito kwa jamii kujenga utamaduni wa kuwajali watoto wanaishi katika mazingira hatarishi na makao ya watoto ili waweze kufikia ndoto zao. “Jukumu la malezi kwa watoto wanaoishi katika makao ya watoto si jukumu la wasimamizi wa vituo pekee, bali ni jukumu la jamii nzima” alisema Hassan.

Akimkaribisha mkuu wa Mkoa wa Iringa, Afisa Wanyamapori katika ofisi ya mkuu wa Mkoa, Hawa Mwechaga alisema kuwa ziara hiyo itatembelea vituo viwili ambayo ni makao ya watoto walio katika mazingira hatarishi. Alisema kuwa lengo la ziara hiyo ni kuonesha upendo, mshikamano na kuwafariji watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi katika majira haya kuelekea sikukuu ya Idi El Fitri. Alisema kuwa zawadi zilizotolewa kwa watoto ni unga, sabuni, mbuzi, mchele, nguo za ndani biscut, pipi, madaftari, peni na nguo kwa ajili ya walezi vyote vikiwa na thamani ya shilingi 1,390,000.

Makao ya watoto ya Dar Bilal yaliyopo eneo la Ilala Manispaa ya Iringa yana watoto 115, kati yao wavulana 55 na wasichana 60.

=30=



Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.