• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

WILAYA YA KILOLO YATAKIWA KUHAMASISHA JAMII KUJENGA MIUNDOMBINU YA ELIMU

Posted on: July 3rd, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Watalaam wa sekta ya elimu wilayani Kilolo wametakiwa kuielimisha na kuihamasisha jamii kuunga mkono juhudi zinazofanywa za kujenga miundombinu ya elimu kwa lengo la kukuza utoaji wa huduma hiyo.

Kauli hiyo ilitolewa na mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alipokuwa akifungua kikao cha wadau wa maendeleo ya sekta ya elimu wilaya ya Kilolo kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri ya wilaya ya Kilolo.

Masenza alisema kuwa shule wilayani Kilolo zinachangamoto ya miundombinu, utoaji wa chakula cha mchana na usimamizi makini wa utekelezaji wa sera ya elimu. “Sote kwa pamoja tunawajibika kuihamasisha jamii juu ya kuchangia maendeleo ya taasisi zetu za kielimu. Jukumu la kuhakikisha shule zetu zina miundombinu madhubuti ni la jamii inayotuzunguka kwa ubia na serikali yetu ya awamu ya tano. Wajibu wetu ni kuielimisha jamii juu ya hili na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na jamii” alisema Masenza. Yapo maeneo ambayo yamefikia mafanikio makubwa, ambayo yanatakiwa mafanikio hayo kuambukizwa maeneo ambayo hayafanyi vizuri, aliongeza.

Mkuu wa Mkoa aliwataka wadau wa maendeleo ya sekta ya elimu wilaya ya Kilolo kuchambua na kushirikishana mipango itakayoleta maendeleo thabiti katika sekta ya elimu. Aidha, aliwataka kujenga ari ya ushindani na kupigania nafasi za ushindani wa juu zaidi katika kufikia mafanikio ya sekta ya elimu. Aliwataka kutumia kikao hicho kuongeza juhudi na ubunifu utakaosaidia kutatua changamoto na kuongeza ufanisi katika kuendeleza sekta ya elimu.

Kikao cha wadau wa sekta ya elimu Wilaya ya Kilolo kinalenga kuwakumbusha wajibu katika kufikia mafanikio ya sekta ya elimu pamoja na kushirikishana changamoto na kujadili suluhisho la pamoja.

=30=


Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.