• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Iringa Region

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Iringa Region

  • Home
  • About Us
    • History
    • Location
    • Vision and Mission
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Administration
    • Organisation Structure
    • Sections
      • Administration and Human Resources
      • Education
      • Planning and Coordination
      • Health and Social Welfare
      • Economic and Production
      • Infrastructure
      • Water Service
      • LGAs Management
    • Units
      • Finance and Accounts
      • Internal Audit
      • Information and Communication Technology
      • Legal Service
      • Procurement Management Unit
  • Districts
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • District
    • Iringa MC
    • Mafinga TC
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Investiment Opportunities
    • Agriculture
    • Livestock
    • Industries and Trade
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Ruaha National Park
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Our Services
    • Health
    • Education
    • Water
    • Agriculture
    • Livestock
    • Fishing
    • Civil Servant Cervices
  • Publications
    • Guidlines
    • Policies
    • News
    • Forms
  • Media Center
    • Photo Gallery
    • Videos
    • News Later
    • Events

ZIARA YA MKUU WA MKOA PAMOJA NA KAMATI YA SIASA MKOA WA IRINGA KUKAGUA MIRADI KATIKA HARMASHAURI YA MANISPAA IRINGA

Posted on: January 19th, 2022

ZIARA YA MKUU WA MKOA PAMOJA NA KAMATI YA SIASA MKOA WA IRINGA KUKAGUA MIRADI KATIKA HARMASHAURI YA MANISPAA IRINGA.

WAKAZI wa kata ya Mkimbizi na maeneo jirani mjini Iringa wanatarajia kuanza kupata huduma za afya kupitia kituo cha Afya Mkimbizi, kinachojengwa katika kata hiyo kwa zaidi ya Sh Milioni 250.

Fedha hizo ni sehemu ya makusanyo ya tozo ya miamala ya simu zilizotolewa na serikali kwa halmashauri ya manispaa ya Iringa ili kuwezesha ujenzi wa kituo hicho katika kata hiyo yenye idadi kubwa ya watu, mjini Iringa.

Mbali na kituo hicho, serikali pia imetoa Sh Milioni 12.5 za tozo hizo kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya Sekondari Ipogolo.

Taarifa ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mh.Queen Sendiga imepongeza ujenzi wa miradi hiyo iliyoelezwa kwamba itasaidia kusogeza huduma za afya karibu na wananchi na kupunguza msongamano wa wanafunzi madarasani.

Kamati ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Iringa ilitembelea miradi hiyo hivikaribuni na kuridhishwa na kasi ya utekelezaji wake.

Wakati mradi wa ujenzi wa kituo cha afya umefikia asilimia 60, madarasa mawili katika shule ya sekondari Ipogolo yamekamilika na tayari yameanza kutumiwa na wanafunzi wa shule hiyo.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk Abel Nyamahanga alisema ujenzi wa majengo hayo (kituo cha afya na madarasa) utasaidia sana katika kuboresha huduma katika manispaa hiyo.

“Tunaanza kuona umuhimu wa tozo kila tunapoona miradi kama hii. Tuna kila sababu ya kuunga mkono mipango ya serikali kwani faida zake ni nyingi na muhimu kwa wananchi wote,” alisema.

Wakati huo huo kamati hiyo imeridhishwa pia na ujenzi wa barabara ya Don Bosco Mawelewele- Zizi na Kitasengwa inayojengwa kwa kiwango cha lami.

Meneja wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tarura) wa wilaya ya Iringa, Barnabas Jabiry alisema wakati barabara ya Donbosco Mawelewele ina urefu wa kilometa moja ya Kitasengwa ni ya kilometa 0.65.

Mbali na kupendezesha mji, Jabiry alisema miradi hiyo itakapokamilika itapunguza adha ya usafiri kwa wakazi wa kata ya Mwangata, Mkwawa na Isakalilo mjini Iringa.

“Kupitika vizuri kwa barabara hizo kutasababisha wananchi husika kuweza kufanya shughuli zao za kijamii na kiuchumi kwa urahisi,” alisema.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Iringa amesema ujenzi wa machinjio ya kisasa ya Ngelewala umefikia zaidi ya asilimia 90.

Mh.Sendiga amesema“matarajio ya mkoa na manispaa ya Iringa ni kuona kwamba machinjio hiyo inaanza kufanya kazi ifikapo Machi mwaka huu.”



Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • MTIHANI MWEMA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • MWENGE WA UHURU 2025 WAKAMILISHA ZIARA MKOA WA IRINGA NA KUKABIDHIWA MKOA WA NJOMBE

    May 03, 2025
  • View All

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
More Videos

Quick Links

  • Iringa Region Revenue Collection
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Related Links

  • State House
  • Public Service Recruitment Secretariat
  • PORALG
  • National Bureau of Statitics
  • Information Department
  • Tanzania Government Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

COUNTER-free

Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Postal Address: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Telephone: +255 262 702 715

    Mobile:

    Email: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2024 Iringa Regional Secretariat. All rights reserved.