• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

MASENZA ATAKA USHIRIKIANO KUFANIKISHA MAONESHO YA UTALII KARIBU KUSINI

Posted on: August 31st, 2017

Mikoa ya nyanda za juu kusini imetakiwa kudumisha umoja katika kufanikisha maonesho ya Utalii Karibu Kusini na shughuli za viwanda vidogo mwaka 2017.

Wito huo umetolewa na mwenyekiti wa kikao cha viongozi wakuu wa mikoa ya nyanda za juu kusini, Amina Masenza alipokuwa akifungua kikao cha pamoja cha maandalizi ya maadhimisho ya maonesho ya Utalii Karibu kusini na maonesho ya shughuli za viwanda vidogo (SIDO) kilichofanyika katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha jana.

Masenza alisema kuwa kanda ya nyanda za juu kusini inatakiwa kujipambanua kupitia utofauti wa kiutalii uliopo. “Tunayo maonesho ya Utalii Karibu Kusini kwa mikoa ya nyanda za juu kusini yatakayofanyika mkoani Iringa. Naomba waheshimiwa wakuu wa mikoa tushikaname kwa dhati ili jambo hili lifanikiwe” alisema Masenza. Aliongeza kuwa ikitokea kiongozi mmoja miongoni mwao akajiondoa atakuwa anaichelewesha kanda ya nyanda za juu kusini kufunguka kimaendeleo kupitia utalii. Alisisitiza kuwa ushirikiano wa pamoja ni msingi imara wa kufanikisha maonesho ya utalii na shughuli za viwanda kwa ukanda huo.

Katika salamu za mkuu wa mkoa wa Songwe, Luteni (Mst) Chiku Galawa alisema kuwa nyanda za juu kusini kuna fursa nyingi na kubwa za kiutalii. “Mwanzo ni mgumu siku zote. Fursa zilizopo ni nyingi na kubwa, kuanzia ziwa Tanganyika, ziwa Rukwa, Hifadhi za Mahale, Katavi, Ruaha, Kitulo, Selous kuna fursa nyingi na tofauti za kitalii” alisema Luteni Galawa. Aliongeza kuwa katika kufikia mafanikio, kazi ya ziada lazima ifanyike. “Ndugu zangu, tunahitaji kujitoa na kuonesha dhamira ya kweli. Lazima fursa tuzitengeneze sisi wenyewe, tusisubiri watu wa nje” alisema Luteni Galawa.

Maadhimisho ya Utalii Karibu Kusini na maonesho ya shughuli za viwanda vigodo (SIDO) yataanza tarehe 29/9/2017-2/10/2017 katika uwanja wa Kichangani- Kihesa Manispaa ya Iringa.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.