• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

MAAFISA ELIMU WAAGIZWA KUSIMAMIA MAENDELEO YA MICHEZO MASHULENI

Posted on: June 29th, 2025

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Dkt. Festo Dugange, ametoa maagizo kwa Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri kuhakikisha wanasimamia kwa ukamilifu maendeleo ya michezo na sanaa mashuleni, kama sehemu ya mkakati wa Serikali wa kukuza vipaji vya wanafunzi kupitia mashindano ya UMITASHUMTA na UMISSETA.

Akizungumza wakati wa kufunga mashindano ya kitaifa ya UMITASHUMTA na UMISSETA yaliyofanyika mkoani Iringa, tarehe 29 Juni 2025, Dkt. Dugange aliwataka maafisa hao kutekeleza maagizo ya Serikali kwa vitendo ili kuimarisha michezo kuanzia ngazi ya shule za msingi hadi Sekondari.

"Maafisa Elimu wa Mikoa na Halmashauri, simamieni kwa nguvu shule za michezo na shule za amali katika maeneo yenu. Hakikisheni mnaweka walimu wenye taaluma ya michezo na sanaa katika shule hizo na kuwawezesha kwa kuwapatia vifaa muhimu vya kufundishia," alisisitiza Dkt. Dugange.

Aidha, alieleza kuwa Mikoa iliyowekeza katika shule maalum za michezo (vitalu) imeonesha mafanikio makubwa kwenye mashindano ya mwaka huu, jambo linalothibitisha kuwa uwekezaji sahihi katika michezo huzaa matokeo chanya.

Kuhusu miundombinu, Dkt. Dugange amebainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imeshaanza kutekeleza mpango wa kuboresha miundombinu ya michezo katika shule teule 56 za Sekondari kwa kujenga na kukarabati viwanja pamoja na ununuzi wa vifaa vya michezo.

"Tathmini tayari imekamilika katika shule saba kutoka mikoa saba, na sasa hatua ya kutangaza zabuni kwa ajili ya kumpata mkandarasi inaendelea," alisema Dkt. Dugange.

Vilevile, alisisitiza umuhimu wa michezo katika maendeleo ya kitaaluma na kijamii kwa wanafunzi, akieleza kuwa michezo hujenga nidhamu, huongeza ujasiri, kuboresha afya na kuchangia ongezeko la mahudhurio shuleni.

Katika hatua nyingine, aliagiza Maafisa Elimu kuhakikisha maeneo ya shule yaliyotengwa kwa ajili ya michezo hayaingiliwi na matumizi mengine, huku akihimiza ushirikiano na wadau wa sekta binafsi katika kuanzisha vituo vya michezo na akademia mashuleni.


Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU ASHIRIKI MBIO ZA GRUMA 2025

    July 05, 2025
  • KUELEKEA MBIO ZA THE GREAT RUAHA MARATHON

    July 01, 2025
  • MAAFISA ELIMU WAAGIZWA KUSIMAMIA MAENDELEO YA MICHEZO MASHULENI

    June 29, 2025
  • MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 YACHAGIZA UCHUMI WA IRINGA.

    June 29, 2025
  • Tazama zote

Video

MAENDELEO KWA SASA BILA MAWASILIANO HAYAWEZEKANI- RC KHERI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.