• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

WANANCHI MUFINDI DC WAIELEWA SERIKALI ELIMU BILA MALIPO- DAS BENARD

Posted on: May 23rd, 2018

Na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Wananchi wa halmashauri ya Wilaya ya Mufindi wameelewa dhana serikali ya awamu ya tano ya utoaji wa elimu bila malipo na kuchangia ujenzi wa miundombinu ya elimu.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Mufindi, Allan Benard alipokuwa akisoma risala ya utii ya wananchi wa halmashauri ya Wilaya ya Mufindi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uwanja wa mkesha wa Mwenge wa uhuru katika Kata ya Igowole, Tarafa ya Kasanga wilayani Mufindi.

Benard alisema kuwa wananchi wameelewa vizuri dhana ya serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais, Dkt John Magufuli ya elimu bila malipo nchini. “Hii inadhihirishwa na ongezeko la wanafunzi wanaoandikishwa kila mwaka, kupungua kwa utoro katika shule za msingi na sekondari, ambapo mahudhurio ya wanafunzi yameongezeka kwa shule za msingi kwa asilimia 96 (2015), asilimia 98 (2018) na sekondari ni asilimia 80 (2015) hadi asilimia 88 (2018)” alisema Benard. Wananchi kushiriki katika ujenzi wa miundombinu mbalimbali ni ishara ya uelewa wa dhana hiyo. “Jumla ya daharia 22 zimejengwa katika shule za sekondari kwa ushirikiano wa wananchi na halmashauri. Pia wananchi kuchangia chakula cha wanafunzi. jumla ya shule 72 za msingi kati ya 147 zinatoa chakula cha mchana na shule 26 za sekondari kati ya shule 33 zinatoa chakula kwa wanafunzi” aliongeza Benard.

Ikumbukwe kuwa tangu kuanza kwa mpango wa elimu bila malipo nchini mwezi Disemba, 2015 hadi mwezi Machi, 2018 halmashauri imepokea jumla ya shilingi 3,015,122,456 kwa ajili ya fidia ya ada, fedha ya chakula kwa wanafunzi wa bweni na ruzuku ya vifaa vya kufundishia na kujifunzia katika shule za sekondari.

=30=

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • ‎RC SERUKAMBA AITAKA TRA KUDHIBITI RISITI FEKI, KUHAMASISHA ELIMU YA KODI

    May 19, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM MKOA WA IRINGA.

    May 18, 2025
  • UKAGUZI WA MIRADI HALMASHAURI YA WILAYA YA MUFINDI

    May 08, 2025
  • RC SERUKAMBA AHIMIZA UWAJIBIKAJI KWA VIONGOZI NA WATUMISHI

    May 07, 2025
  • Tazama zote

Video

RC SERUKAMBA: WANANCHI PAWAGA FANYENI KAZI KWA BIDII.
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.