• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Iringa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Iringa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Mahala
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Elimu
      • Mipango na Uratibu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Huduma ya Maji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Tehama
      • Huduma za Kisheria
      • Manunuzi na Ugavi
  • Wilaya
    • Iringa
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Mufindi
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
    • Kilolo
      • Historia
      • Viongozi
      • Halmashauri zilizopo kwenye Wilaya
  • Halmashauri
    • Iringa MC
    • Mafinga Mji
    • Iringa DC
    • Kilolo DC
    • Mufindi DC
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Viwanda na Biashara
    • Vivutio vya Kitalii
      • Fahari Yetu
      • CHOGELASAFARICAMP
      • Kitovu cha Utalii Nyanda za Juu Kusini
      • RUAHA HILLTOP
      • Hifadhi ya Taifa Ruaha
      • Udzungwa Mountains National Park
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sera
    • Habari
    • Fomu
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • News Later
    • Matukio

MAMA SAMIA ASIKITISHWA NA WAPINGA MAENDELEO IRINGA

Posted on: February 11th, 2018

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa

Makamu wa Rais wa Tanzania, mama Samia Suluhu Hassan amesikitishwa na watu wanaokwamisha juhudi za wananchi kujiletea maendeleo na kuuagiza uongozi wa Mkoa wa Iringa kuwachukulia hatua kwa mujibu wa sheria.

Mama Hassan alionesha masikitiko yake jana alipokuwa akihutubia mamia ya wananchi wa mji mdogo wa Ilula na vitongoji vyake jana.

Mama Hassan alisema kuwa wapo watu wanaopita mitaani kudumaza kasi ya maendeleo na nguvu za wananchi zinazowekwa katika kujiletea maendeleo. Aliongeza kuwa wapo wafanyabiashara na sekta binafsi wameonesha nguvu zao katika kuunga mkono juhudu za wananchi kuwaletea maendeleo lakini wanakwamishwa na baadhi ya watu kutofikia dhamira ya serikali. “Watu hao wanaodumaza juhudi za maendeleo wanajiita watanzania. Naomba sana kama kuna watu wa aina hiyo, washughulikieni. Sheria, kanuni na miongozo ipo. Hapana hatuwezi kuendelea kwa namna hiyo” alisema mama Hassan.

Akitoa salamu za Rais Dr. John Magufuli, Makamu wa Rais alisema kuwa “Mheshimiwa Rais anawapongeza wananchi wa Kilolo kwa juhudi wanazozifanya kujiletea maendeleo. Anaelewa juhudi mnazozifanya katika kujenga hospitali ya wilaya na hatua mliyofikia. Anaipongeza wilaya kwa kupata hati safi ya hesabu za serikali kwa mwaka wa fedha 2015/2016” alisema mama Hassan.

Makamu wa Rais aliwataka wananchi wa Kilolo kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais Dr. Magufuli na serikali yake ya awamu ya tano kwa kufanya kazi kwa bidii ili maendeleo yaende kwa kasi. Serikali itasukuma sekta za elimu, afya, maji, umeme vijijini na miundombinu ili huduma hizo ziwe rahisi kwa wananchi na kuwaongezea kasi ya kufanya kazi.

=30=



Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • KUELEKEA MBIO ZA THE GREAT RUAHA MARATHON

    July 01, 2025
  • MAAFISA ELIMU WAAGIZWA KUSIMAMIA MAENDELEO YA MICHEZO MASHULENI

    June 29, 2025
  • MASHINDANO YA UMITASHUMTA NA UMISSETA 2025 YACHAGIZA UCHUMI WA IRINGA.

    June 29, 2025
  • KARIBU MKOANI IRINGA

    June 28, 2025
  • Tazama zote

Video

MAENDELEO KWA SASA BILA MAWASILIANO HAYAWEZEKANI- RC KHERI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Iringa
  • PReM
  • Investment profile
  • Ajira za waalimu
  • Press release

Tovuti Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu (NBS)
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji Kidunia

world map hits counter

Jumla ya Watembeleaji

COUNTER-free

Ramani

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 4 Barabara ya Pawaga

    Anuani ya Posta: P.O.Box 858, 51108 Gangilonga, Iringa, Tanzania

    Simu: +255 262 702 715

    Mobile:

    Barua pepe: ras@iringa.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali
    • Ramani
    • Huduma

Hakimiliki ©2025, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Iringa.